1. Heri yake mtu aliyesamehewa kosa lake,mtu ambaye dhambi yake imeondolewa kabisa.
2. Heri mtu ambaye Mwenyezi-Mungu hamwekei hatia,mtu ambaye hana hila moyoni mwake.
3. Wakati nilipokuwa sijakiri dhambi yangu,nilikuwa nimedhoofika kwa kulia mchana kutwa.
4. Mchana na usiku mkono wako ulinilemea;nikafyonzwa nguvu zangu,kama maji wakati wa kiangazi.
5. Kisha nilikiri makosa yangu kwako;wala sikuuficha uovu wangu.Nilisema ninakuungamia makosa yangu ee Mwenyezi-Mungu,ndipo nawe ukanisamehe dhambi zangu zote.
6. Kwa hiyo, kila mwaminifu na akuletee maombi;jeshi likaribiapo au mafuriko,hayo hayatamfikia yeye.
7. Wewe ndiwe kinga yangu;wewe wanilinda katika taabu.Umenijalia shangwe za kukombolewa.
8. Mungu asema: “Nitakufunzana kukuonesha njia unayopaswa kufuata.Nitakushauri kwa uangalifu mkubwa.
9. Usiwe mpumbavu kama farasi au nyumbu,ambao lazima wafungwe lijamu na hatamu,la sivyo hawatakukaribia.”
10. Watu waovu watapata mateso mengi,bali wanaomtumainia Mwenyezi-Mungu wazungukwa na fadhili zake.
11. Furahini na kushangilia kwa sababu ya Mwenyezi-Mungu enyi waadilifu;pigeni vigelegele vya shangwe enyi wanyofu wa moyo.