Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 29 Biblia Habari Njema (BHN)

Sauti ya Mungu katika dhoruba

(Zaburi ya Daudi)

1. Mpeni Mwenyezi-Mungu heshima enyi viumbe vya mbinguni,semeni Mwenyezi-Mungu ni mtukufu na mwenye nguvu.

2. Semeni jina la Mwenyezi-Mungu ni tukufu.Mwabuduni katika mahali pake patakatifu.

3. Sauti ya Mwenyezi-Mungu yasikika juu ya maji;Mungu mtukufu angurumisha radi,sauti ya Mwenyezi-Mungu yasikika juu ya bahari!

4. Sauti ya Mwenyezi-Mungu ina nguvu,sauti ya Mwenyezi-Mungu imejaa fahari.

5. Sauti ya Mwenyezi-Mungu huvunja mierezi;Mwenyezi-Mungu avunja mierezi ya Lebanoni.

6. Huirusha milima ya Lebanoni kama ndama,milima ya Sirioni kama mwananyati.

7. Sauti ya Mwenyezi-Mungu hutoa miali ya moto.

8. Sauti ya Mwenyezi-Mungu hutetemesha jangwa,Mwenyezi-Mungu hutetemesha jangwa la Kadeshi.

9. Sauti ya Mwenyezi-Mungu huitikisa mivule,hukwanyua majani ya miti msituni,na hekaluni mwake wote wasema:“Utukufu kwa Mungu!”

10. Mwenyezi-Mungu ameketi juu ya gharika;Mwenyezi-Mungu ni mfalme atawalaye milele.

11. Mwenyezi-Mungu na awape watu wake nguvu!Mwenyezi-Mungu na awabariki watu wake kwa amani!