1. Ee Mungu mtetezi wa haki yangu, unijibu niombapo.Nilipokuwa katika shida, wewe ulinisaidia;unionee huruma na kusikia sala yangu.
2. Jamani, mtaniharibia jina langu mpaka lini?Mpaka lini mtapenda upuuzi na kusema uongo?
3. Jueni kuwa Mwenyezi-Mungu amejiteulia mwaminifu wake.Mwenyezi-Mungu husikia kila ninapomwomba.
4. Tetemekeni kwa hofu na msitende dhambi;tafakarini vitandani mwenu na kunyamaza.
5. Toeni tambiko zilizo sawa,na kumtumainia Mwenyezi-Mungu.
6. Wengi husema: “Laiti tungepata tena fanaka!Utuangalie kwa wema, ee Mwenyezi-Mungu!”
7. Lakini mimi umenijalia furaha kubwa moyoni,kuliko ya hao walio na divai na ngano kwa wingi.
8. Nalala na kupata usingizi kwa amani;ee Mwenyezi-Mungu, wewe peke yako waniweka salama.