Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 4 Biblia Habari Njema (BHN)

Kuomba msaada jioni

(Kwa Mwimbishaji: Na ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Daudi)

1. Ee Mungu mtetezi wa haki yangu, unijibu niombapo.Nilipokuwa katika shida, wewe ulinisaidia;unionee huruma na kusikia sala yangu.

2. Jamani, mtaniharibia jina langu mpaka lini?Mpaka lini mtapenda upuuzi na kusema uongo?

3. Jueni kuwa Mwenyezi-Mungu amejiteulia mwaminifu wake.Mwenyezi-Mungu husikia kila ninapomwomba.

4. Tetemekeni kwa hofu na msitende dhambi;tafakarini vitandani mwenu na kunyamaza.

5. Toeni tambiko zilizo sawa,na kumtumainia Mwenyezi-Mungu.

6. Wengi husema: “Laiti tungepata tena fanaka!Utuangalie kwa wema, ee Mwenyezi-Mungu!”

7. Lakini mimi umenijalia furaha kubwa moyoni,kuliko ya hao walio na divai na ngano kwa wingi.

8. Nalala na kupata usingizi kwa amani;ee Mwenyezi-Mungu, wewe peke yako waniweka salama.