Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 27 Biblia Habari Njema (BHN)

Kwa Mungu kuna usalama

(Zaburi ya Daudi)

1. Mwenyezi-Mungu ni mwanga wangu na wokovu wangu,ni nani nitakayemwogopa?Mwenyezi-Mungu ni ngome ya maisha yangu,sitamwogopa mtu yeyote.

2. Waovu wakinishambulia,na kutaka kuniangamiza,hao wapinzani wangu watajikwaa na kuanguka.

3. Hata jeshi likinizunguka,moyo wangu hautaogopa kitu;hata nikikabiliwa na vita,bado nitakuwa na tumaini.

4. Jambo moja nimemwomba Mwenyezi-Mungu,nalo ndilo ninalolitafuta:Nikae nyumbani mwa Mwenyezi-Mungusiku zote za maisha yangu;niuone uzuri wake Mwenyezi-Mungu,na kutafuta maongozi yake hekaluni mwake.

5. Siku ya taabu atanificha bandani mwake;atanificha katika hema lake,na kunisalimisha juu ya mwamba.

6. Nami kwa fahari nitaangalia juuya maadui zangu wanaonizunguka.Nitamtolea tambiko kwa shangwe hekaluni mwake,nitaimba na kumshangilia Mwenyezi-Mungu.

Msaada wapatikana kwa Mungu

7. Usikie, ee Mwenyezi-Mungu, ninapokulilia,unionee huruma na kunijibu.

8. Moyo wangu waniambia: “Njoo umtafute Mungu!”Basi, naja kwako, ee Mwenyezi-Mungu.

9. Usiache kuniangalia kwa wema.Usinikatae kwa hasira mimi mtumishi wako;wewe umekuwa daima msaada wangu.Usinitupe wala usiniache, ee Mungu Mwokozi wangu.

10. Hata kama wazazi wangu wakinitupa,Mwenyezi-Mungu atanipokea kwake.

11. Unifundishe njia yako, ee Mwenyezi-Mungu;uniongoze katika njia iliyo sawa,kwa sababu ya maadui zangu.

12. Usiniache maadui wanitende wapendavyo;maana mashahidi wa uongo wananikabili,nao wanatoa vitisho vya ukatili.

13. Naamini nitauona wema wake Mwenyezi-Mungukatika makao ya walio hai.

14. Mtegemee Mwenyezi-Mungu!Uwe na moyo, usikate tamaa!Naam, mtegemee Mwenyezi-Mungu!