Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 14 Biblia Habari Njema (BHN)

Uovu wa watu

(Kwa Mwimbishaji. Zaburi ya Daudi)

1. Wapumbavu hujisemea moyoni:“Hakuna Mungu.”Wote wamepotoka kabisa,wametenda mambo ya kuchukiza;hakuna hata mmoja atendaye jema!

2. Mwenyezi-Mungu anawaangalia wanadamu kutoka mbinguni,aone kama kuna yeyote mwenye busara,kama kuna yeyote anayemtafuta Mungu.

3. Lakini wote wamekosa,wote wamepotoka pamoja;hakuna atendaye mema,hakuna hata mmoja.

4. “Je, hao watendao maovu hawana akili?Wanawatafuna watu wangu kama mikate;wala hawanijali mimi Mwenyezi-Mungu.”

5. Hapo watashikwa na hofu kubwa,maana Mungu yu pamoja na waadilifu.

6. Unaweza kuvuruga mipango ya maskini,lakini Mwenyezi-Mungu ndiye kimbilio lake.

7. Laiti ukombozi wa Israeli ungefika kutoka Siyoni!Mwenyezi-Mungu atakaporekebisha hali ya watu wake,wazawa wa Yakobo watashangilia;Waisraeli watafurahi.