Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 8 Biblia Habari Njema (BHN)

Utukufu wa Mungu na cheo cha binadamu

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo wa Gitithi. Zaburi ya Daudi)

1. Ee Mwenyezi-Mungu, Bwana wetu,kweli jina lako latukuka duniani kote!Utukufu wako waenea mpaka juu ya mbingu!

2. Kwa sifa za watoto wadogo na wanyonyao,umejiwekea ngome dhidi ya adui zako,uwakomeshe waasi na wapinzani wako.

3. Nikiangalia mbingu, kazi ya vidole vyako,mwezi na nyota ulizozisimika huko,

4. mtu ni nini, ee Mungu, hata umfikirie,binadamu ni nini hata umjali?

5. Umemfanya awe karibu kama Mungu,umemvika fahari na heshima.

6. Ulimpa madaraka juu ya kazi zako zote;uliviweka viumbe vyote chini ya mamlaka yake:

7. Kondoo, ng'ombe, na wanyama wa porini;

8. ndege, samaki, na viumbe vyote vya baharini.

9. Ee Mwenyezi-Mungu, Bwana wetu,kweli jina lako latukuka duniani kote!