1. Fanya haraka, ee Mwenyezi-Mungu!Watu wema wamekwisha;waaminifu wametoweka miongoni mwa watu.
2. Kila mmoja humdanganya mwenzake,husema kwa kudanganya na kwa moyo wa unafiki.
3. Ee Mwenyezi-Munguuikomeshe hiyo midomo ya udanganyifu,na ndimi hizo zinazojigamba kupindukia.
4. Wao husema: “Kwa ndimi zetu tutashinda;midomo tunayo, nani awezaye kututawala?”
5. Lakini Mwenyezi-Mungu asema:“Kwa sababu maskini wanadhulumiwa,na wahitaji wanapiga kite, sasa naja,nami nitawapa usalama wanaoutazamia.”
6. Neno la Mwenyezi-Mungu ni safi,safi kama fedha iliyosafishwa katika tanuri,naam, kama fedha iliyosafishwa mara saba.
7. Utulinde, ee Mwenyezi-Mungu,utukinge daima na kizazi hiki kiovu.
8. Waovu wanazunguka kila mahali;upotovu unatukuzwa kati ya watu.