Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 12 Biblia Habari Njema (BHN)

Kuomba msaada

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo wa Sheminithi. Zaburi ya Daudi)

1. Fanya haraka, ee Mwenyezi-Mungu!Watu wema wamekwisha;waaminifu wametoweka miongoni mwa watu.

2. Kila mmoja humdanganya mwenzake,husema kwa kudanganya na kwa moyo wa unafiki.

3. Ee Mwenyezi-Munguuikomeshe hiyo midomo ya udanganyifu,na ndimi hizo zinazojigamba kupindukia.

4. Wao husema: “Kwa ndimi zetu tutashinda;midomo tunayo, nani awezaye kututawala?”

5. Lakini Mwenyezi-Mungu asema:“Kwa sababu maskini wanadhulumiwa,na wahitaji wanapiga kite, sasa naja,nami nitawapa usalama wanaoutazamia.”

6. Neno la Mwenyezi-Mungu ni safi,safi kama fedha iliyosafishwa katika tanuri,naam, kama fedha iliyosafishwa mara saba.

7. Utulinde, ee Mwenyezi-Mungu,utukinge daima na kizazi hiki kiovu.

8. Waovu wanazunguka kila mahali;upotovu unatukuzwa kati ya watu.