Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 34 Biblia Habari Njema (BHN)

Sifa kwa wema wa Mungu

(Zaburi ya Daudi alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki)

1. Nitamtukuza Mwenyezi-Mungu nyakati zote,sitaacha kamwe kuzitamka sifa zake.

2. Mimi nitaona fahari juu ya Mwenyezi-Mungu,wanyonge wasikie na kufurahi.

3. Mtukuzeni Mwenyezi-Mungu pamoja nami,sote pamoja tulisifu jina lake.

4. Nilimwomba Mwenyezi-Mungu naye akanijibu,na kuniondoa katika hofu zangu zote.

5. Mgeukieni Mungu mpate kufurahi;nanyi hamtaaibishwa kamwe.

6. Maskini alimlilia Mwenyezi-Mungu, naye akamsikia,na kumwokoa katika taabu zake zote.

7. Malaika wa Mwenyezi-Mungu huwalinda wote wamchao,na kuwaokoa katika hatari.

8. Jaribuni mwone Mwenyezi-Mungu alivyo mwema.Heri mtu anayekimbilia usalama kwake.

9. Mcheni Mwenyezi-Mungu enyi watakatifu wake;maana wenye kumcha hawatindikiwi na kitu.

10. Hata wanasimba hutindikiwa na kuona njaa;lakini wanaomtafuta Mwenyezi-Mungu hawakosi chochote chema.

11. Njoni enyi vijana mkanisikilize,nami nitawafundisha kumcha Mwenyezi-Mungu.

12. Je, watamani kufurahia maisha,kuishi maisha marefu na kufurahia mema?

13. Basi, acha kusema mabaya,na kuepa kusema uongo.

14. Jiepushe na uovu, utende mema;utafute amani na kuizingatia.

15. Mwenyezi-Mungu huwaangalia waadilifu,na kusikiliza malalamiko yao;

16. lakini huwapinga watu watendao maovu,awafutilie mbali kutoka duniani.

17. Waadilifu wakimlilia Mwenyezi-Mungu yeye huwasikia,na kuwaokoa katika taabu zao zote.

18. Mwenyezi-Mungu yu karibu na waliokufa moyo;huwaokoa wote waliokata tamaa kabisa.

19. Mateso ya mwadilifu ni mengi,lakini Mwenyezi-Mungu humwokoa kutoka yote.

20. Huvilinda viungo vya mwili wake wote,hakuna hata mfupa wake mmoja utakaovunjwa.

21. Ubaya huwaletea waovu kifo;wanaowachukia waadilifu wataadhibiwa.

22. Mwenyezi-Mungu huokoa maisha ya watumishi wake,wote wanaomkimbilia hawataadhibiwa.