Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 30 Biblia Habari Njema (BHN)

Sala ya shukrani

(Zaburi ya Daudi)

1. Ee Mwenyezi-Mungu, nakutukuza maana umeniokoa,wala hukuwaacha maadui zangu wanisimange.

2. Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu,nilikulilia msaada, nawe ukaniponya.

3. Ee Mwenyezi-Mungu, umeniokoa kutoka kuzimu;umenipa tena uhai,umenitoa miongoni mwa waendao kuzimu.

4. Mwimbieni Mwenyezi-Mungu sifa, enyi waaminifu wake;kumbukeni utakatifu wake na kumshukuru.

5. Hasira yake hudumu kitambo kidogo,wema wake hudumu milele.Kilio chaweza kuwapo hata usiku,lakini asubuhi huja furaha.

6. Mimi nilipofanikiwa, nilisema:“Kamwe sitashindwa!”

7. Kwa wema wako, ee Mwenyezi-Mungu,umeniimarisha kama mlima mkubwa.Lakini ukajificha mbali nami,nami nikafadhaika.

8. Nilikulilia wewe, ee Mwenyezi-Mungu;naam niliomba dua kwako ee Mwenyezi-Mungu:

9. “Je, utapata faida gani nikifana kushuka hadi kwa wafu?Je, mavumbi ya wafu yanaweza kukusifu?Je, yanaweza kusimulia uaminifu wako?

10. Usikie, ee Mwenyezi-Mungu, unihurumie;ee Mwenyezi-Mungu, unisaidie!”

11. Wewe umegeuza maombolezo langu kuwa ngoma ya furaha;umeniondolea huzuni yangu, ukanizungushia furaha.

12. Mimi nitakusifu wala sitakaa kimya.Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu nitakushukuru milele.