Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 10 Biblia Habari Njema (BHN)

Sala dhidi ya udhalimu

1. Ee Mwenyezi-Mungu, mbona wasimama mbali?Kwa nini wajificha wakati tumo taabuni?

2. Kwa kiburi waovu wanawatesa maskini;njama zao ziwanase wao wenyewe.

3. Mwovu hujisifia tamaa zake mbaya,mtu wa tamaa hulaani na kumkataa Mwenyezi-Mungu.

4. Katika majivuno yake husema: “Mungu hatagundua.”Mawazo yake yote ni: “Hakuna Mungu.”

5. Njia za mwovu hufanikiwa daima;kwake hukumu zako ziko mbali na mawazo yake,na huwadharau maadui zake wote.

6. Huwaza moyoni: “Sitakuwa na wasiwasi;sitapatwa na dhiki maishani.”

7. Kinywa chake kimejaa laana, udanganyifu na dhuluma;mwepesi kusema maneno ya kuchukiza na maovu.

8. Hujificha vijijini huku anaotea,amuue kwa siri mtu asiye na hatia.Yuko macho kumvizia mnyonge;

9. huotea mafichoni mwake kama simba.Huvizia apate kuwakamata maskini;huwanasa kwa mtego wake na kuwachukua.

10. Mnyonge huvamiwa na kuangushwa chini;huangushwa kwa ukatili wa mtu mwovu.

11. Mwovu huwaza moyoni mwake: “Mungu amesahau;ameficha uso wake, haoni kitu!”

12. Inuka, ee Mwenyezi-Mungu, uwaadhibu;usiwasahau wanaodhulumiwa.

13. Ee Mungu, kwa nini mwovu anakudharau,na kusema ati hutamfanya awajibike?

14. Lakini wewe wawaona wenye dhiki na shida;nawe daima uko tayari kuwasaidia.Mnyonge anakutegemea wewe, ee Mungu,wewe umekuwa daima msaada wa yatima.

15. Uzivunje nguvu za mtu mwovu;ukomeshe uovu wake wote, usiwepo tena.

16. Mwenyezi-Mungu ni mfalme milele na milele!Mataifa yasiyomjua yatatoweka nchini mwake.

17. Ee Mwenyezi-Mungu, wapokea dua za mnyonge;wampa moyo na kumtegea sikio.

18. Utawatendea haki yatima na wanaodhulumiwa,binadamu aliye udongo asiweze tena kuleta hofu.