Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 25 Biblia Habari Njema (BHN)

Kumwomba Mungu uongozi na ulinzi

(Zaburi ya Daudi)

1. Ee Mwenyezi-Mungu, kwako naielekeza nafsi yangu!

2. Nakutumainia wewe, ee Mungu wangu,usiniache niaibike;adui zangu wasifurahie kushindwa kwangu.

3. Usimwache anayekutumainia apate aibu;lakini waaibike wote wanaokuasi kwa makusudi.

4. Unijulishe njia zako, ee Mwenyezi-Mungu;unifundishe nifuate unayotaka.

5. Uniongoze katika ukweli wako na kunifundisha,kwani wewe ni Mungu, mwokozi wangu;ninakutegemea wewe kila siku.

6. Uikumbuke huruma yako ee Mwenyezi-Mungu;uzikumbuke na fadhili zako kuu,ambazo zimekuwako tangu kale.

7. Usikumbuke dhambi na makosa ya ujana wangu;unikumbuke kadiri ya fadhili zako,kwa ajili ya wema wako, ee Mwenyezi-Mungu.

8. Mwenyezi-Mungu ni mwema na mnyofu,kwa hiyo huwafundisha wenye dhambi njia.

9. Huwaongoza wanyenyekevu katika uadilifu;naam, huwafundisha hao njia yake.

10. Mwenyezi-Mungu hutenda kwa fadhili na uaminifu,kwa wale wanaoshika agano lake na maamuzi yake.

11. Kwa ajili ya jina lako, ee Mwenyezi-Mungu,unisamehe kosa langu kwani ni kubwa.

12. Kila mtu anayemcha Mwenyezi-Mungu,Mwenyezi-Mungu atamfunza njia ya kufuata.

13. Mtu wa namna hiyo atafanikiwa daima,na wazawa wake watamiliki nchi.

14. Mwenyezi-Mungu ni rafiki ya wale wamchao;yeye huwajulisha hao agano lake.

15. Namwangalia Mwenyezi-Mungu daima;yeye atainasua miguu yangu mtegoni.

16. Unielekee, ee Mungu, unionee huruma,maana mimi ni mpweke na mnyonge.

17. Uniondolee mahangaiko ya moyoni mwangu;unitoe katika mashaka yangu.

18. Uangalie mateso yangu na dhiki yangu;unisamehe dhambi zangu zote.

19. Angalia jinsi walivyo wengi maadui zangu;ona jinsi wanavyonichukia kwa ukatili.

20. Uyalinde maisha yangu, uniokoe;nakimbilia usalama kwako,usikubali niaibike.

21. Wema na uadilifu vinihifadhi,maana ninakutumainia wewe.

22. Ee Mungu, uwaokoe watu wako, Israeli;uwaokoe katika taabu zao zote.