Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 24 Biblia Habari Njema (BHN)

Mfalme Mkuu

(Zaburi ya Daudi)

1. Dunia na vyote vilivyomo ni vyake Mwenyezi-Mungu;ulimwengu na wote waishio humo ni mali yake.

2. Maana yeye aliweka misingi ya dunia juu ya bahari;aliisimika imara juu ya mito ya maji.

3. Nani atakayepanda mlima wa Mwenyezi-Mungu?Nani atakayekaa katika hekalu lake takatifu?

4. Ni mtu wa matendo mema na moyo safi,asiyeuelekeza moyo wake katika upuuzi,wala kuapa kwa uongo.

5. Mtu huyo atapokea baraka kwa Mwenyezi-Mungu,na haki yake kwa Mungu mwokozi wake.

6. Ndio hali ya kizazi cha watu wamtafutao yeye;naam, watu wamtafutao Mungu wa Yakobo.

7. Fungukeni enyi milango;fungukeni enyi milango ya kale,ili Mfalme mtukufu aingie.

8. Ni nani huyo Mfalme mtukufu?Ni Mwenyezi-Mungu, mwenye nguvu na uwezo;Mwenyezi-Mungu, mwenye uwezo vitani.

9. Fungukeni enyi malango,fungukeni enyi milango ya kale,ili Mfalme mtukufu aingie.

10. Ni nani huyo Mfalme mtukufu?Ni Mwenyezi-Mungu, wa majeshi,yeye ndiye Mfalme mtukufu.