Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 33 Biblia Habari Njema (BHN)

Utenzi wa kumsifu Mungu

1. Shangilieni kwa sababu ya Mwenyezi-Mungu enyi waadilifu!Kumsifu Mungu ni wajibu wa watu wanyofu.

2. Msifuni Mwenyezi-Mungu kwa zeze;mwimbieni kwa kinubi cha nyuzi kumi.

3. Mwimbieni wimbo mpya;pigeni kinubi vizuri na kushangilia.

4. Neno la Mwenyezi-Mungu ni la kweli;na matendo yake yote ni ya kuaminika.

5. Mungu apenda uadilifu na haki,dunia imejaa fadhili za Mwenyezi-Mungu.

6. Mbingu ziliumbwa kwa neno la Mwenyezi-Mungu,na vyote vilivyomo kwa pumzi ya mdomo wake.

7. Alikusanya maji ya bahari kama katika chupa,vilindi vya bahari akavifunga ghalani.

8. Dunia yote na imwogope Mwenyezi-Mungu!Wakazi wote duniani, wamche!

9. Maana alisema na ulimwengu ukawako;alitoa amri nao ukajitokeza.

10. Mwenyezi-Mungu hupangua mipango ya mataifa,na kuyatangua mawazo yao.

11. Mpango wa Mwenyezi-Mungu hudumu milele;maazimio yake yadumu vizazi vyote.

12. Heri taifa ambalo Mungu wake ni Mwenyezi-Mungu;heri wale aliowachagua kuwa watu wake mwenyewe!

13. Mwenyezi-Mungu huangalia chini kutoka mbinguni,na kuwaona wanadamu wote.

14. Kutoka kwenye kiti chake cha enzi,huwaangalia wakazi wote wa dunia.

15. Yeye huunda mioyo ya watu wote,yeye ajua kila kitu wanachofanya.

16. Mfalme hawezi kuokolewa kwa kuwa na jeshi kubwa;wala shujaa hapati ushindi kwa nguvu zake kubwa.

17. Farasi wa vita hafai kitu kwa kupata ushindi;nguvu zake nyingi haziwezi kumwokoa mtu.

18. Mwenyezi-Mungu huwaangalia wale wamchao,watu ambao wanatumainia fadhili zake.

19. Yeye huwaokoa katika kifo,huwaweka hai wakati wa njaa.

20. Mioyo yetu yamtumainia Mwenyezi-Mungu.Yeye ni msaada wetu na ngao yetu.

21. Naam twafurahi kwa sababu yake;tuna matumaini katika jina lake takatifu.

22. Fadhili zako zikae nasi, ee Mwenyezi-Mungu,kwani sisi tumekuwekea tumaini letu.