Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 36 Biblia Habari Njema (BHN)

Uovu wa binadamu

(Kwa Mwimbishaji. Zaburi ya Daudi, mtumishi wa Mwenyezi-Mungu)

1. Dhambi huongea na mtu mwovu,ndani kabisa moyoni mwake;jambo la kumcha Mungu halimo kabisa kwake.

2. Mwovu hujipendelea mwenyewe,hufikiri uovu wake hautagunduliwa na kulaaniwa.

3. Kila asemacho ni uovu na uongo;ameacha kutumia hekima na kutenda mema.

4. Alalapo huwaza kutenda maovu,hujiweka katika njia isiyo njema,wala haachani na uovu.

Wema wa Mungu

5. Fadhili zako ee Mwenyezi-Mungu zaenea hata mbinguni;uaminifu wako wafika mawinguni.

6. Uadilifu wako ni kama milima mikubwa,hukumu zako ni kama vilindi vya bahari.Wewe, ee Mwenyezi-Mungu, wawalinda wanadamu na wanyama

7. Jinsi gani zilivyo bora fadhili zako!Wanadamu hukimbilia kivulini mwa mabawa yako.

8. Wawashibisha kwa utajiri wa nyumba yako;wawanywesha kutoka mto wa wema wako.

9. Wewe ndiwe asili ya uhai;kwa mwanga wako twaona mwanga.

10. Uendelee kuwafadhili wale wanaokutambua;uzidi kuwa mwema kwa wanyofu wa moyo.

11. Usikubali wenye majivuno wanivamie,wala watu waovu wanikimbize.

12. Kumbe watendao maovu wameanguka;wameangushwa chini, hawawezi kuinuka.