Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 38 Biblia Habari Njema (BHN)

Sala katika mateso

(Zaburi ya Daudi ya matoleo)

1. Ee Mwenyezi-Mungu, usinikemee kwa hasira yako;usiniadhibu kwa ghadhabu yako.

2. Mishale yako imenichoma;mkono wako umenigandamiza.

3. Hamna mahali nafuu mwilini mwangu,kwa sababu umenikasirikia;hamna penye afya hata mifupani mwangu,kwa sababu ya dhambi yangu.

4. Nimefunikwa kabisa na dhambi zangu,zinanilemea kama mzigo mzito mno kwangu.

5. Madonda yangu yameoza na kunuka,na hayo ni matokeo ya ujinga wangu.

6. Nimepindika mpaka chini na kupondeka;mchana kutwa nazunguka nikiomboleza.

7. Viungo vyangu vimeshambuliwa na homa;mwilini mwangu hamna nafuu yoyote.

8. Nimelegea na kupondekapondeka;nasononeka kwa kusongwa moyoni.

9. Ee Bwana, wewe wajua tazamio langu lote;kwako hakikufichika kilio changu.

10. Moyo wanidunda, nguvu zimeniishia;hata macho yangu nayo yamekwisha fifia.

11. Rafiki na wenzangu wanaepa kuona mateso yangu,na jamaa zangu wanakaa mbali nami.

12. Wanaotaka kuniua wanatega mitego yao;wanaonitakia niumie wanatishia kuniangamiza.Mchana kutwa wanafanya mipango dhidi yangu.

13. Lakini mimi nimekuwa kama kiziwi, sisikii;nimekuwa kama bubu asiyeweza kusema kitu.

14. Naam, nimekuwa kama mtu asiyesikia,kama mtu asiye na chochote cha kujitetea.

15. Lakini ninakutumainia wewe, ee Mwenyezi-Mungu;wewe, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, ndiwe utakayenijibu.

16. Nakuomba tu maadui wasinisimange,wasione fahari juu ya kuanguka kwangu.

17. Karibu sana nitaanguka;nakabiliwa na maumivu ya daima.

18. Naungama uovu wangu;dhambi zangu zanisikitisha.

19. Maadui zangu hawajambo, wana nguvu;ni wengi mno hao wanaonichukia bure.

20. Hao wanaonilipa maovu kwa wema wangu,wananipinga kwa sababu natenda mema.

21. Usinitupe, ee Mwenyezi-Mungu;ee Mungu wangu, usikae mbali nami.

22. Uje haraka kunisaidia;ewe Mwenyezi-Mungu, uliye wokovu wangu.