Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 40 Biblia Habari Njema (BHN)

Utenzi wa sifa

(Kwa Mwimbishaji. Zaburi ya Daudi)

1. Nilimngojea Mwenyezi-Mungu kwa uvumilivu,akanielekea na kukisikia kilio changu.

2. Aliniondoa katika shimo la hatari,alinitoa katika matope ya dimbwi,akanisimamisha salama juu ya mwamba,na kuziimarisha hatua zangu.

3. Alinifundisha wimbo mpya,wimbo wa sifa kwa Mungu wetu.Wengi wataona na kuogopa,na kumtumainia Mwenyezi-Mungu.

4. Heri mtu anayemtumainia Mwenyezi-Mungu;mtu asiyejiunga na watu wenye majivuno,watu waliopotoka kwa kuabudu miungu ya uongo.

5. Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, umetufanyia mengi ya ajabu,na mipango yako juu yetu haihesabiki;hakuna yeyote aliye kama wewe.Kama ningeweza kusimulia hayo yote,idadi yake ingenishinda.

6. Wewe hutaki tambiko wala sadaka,tambiko za kuteketeza wala za kuondoa dhambi;lakini umenipa masikio nikusikie.

7. Ndipo niliposema: “Niko tayari;ninayotakiwa kufanya yameandikwa katika kitabu cha sheria;

8. kutimiza matakwa yako, ee Mungu wangu ni furaha yangu,sheria yako naishika kwa moyo wangu wote!”

9. Nimesimulia habari njema za ukombozi,mbele ya kusanyiko kubwa la watu.Kama ujuavyo ee Mwenyezi-Mungu,mimi sikujizuia kuitangaza.

10. Sikuuficha moyoni mwangu ukombozi ulionijalia,nimetangaza daima kuwa wewe ni mwokozi mwaminifu;sikulificha kusanyiko kubwa la watufadhili zako na uaminifu wako.

11. Ee Mwenyezi-Mungu, usininyime huruma yako!Fadhili zako na uaminifu wako vinihifadhi daima.

Sala ya kuomba msaada

12. Maafa yasiyohesabika yanizunguka,maovu yangu yanikaba hata siwezi kuona;ni mengi kuliko nywele kichwani mwangu,nami nimevunjika moyo.

13. Upende ee Mwenyezi-Mungu kuniokoa;ee Mwenyezi-Mungu, uje haraka kunisaidia.

14. Wanaonuia kuniangamiza,na waaibike na kufedheheka!Hao wanaotamani niumie,na warudi nyuma na kuaibika!

15. Hao wanaonisimanga,na wapumbazike kwa kushindwa kwao!

16. Lakini wote wale wanaokutafutawafurahi na kushangilia kwa sababu yako.Wapendao wokovu wako,waseme daima: “Mwenyezi-Mungu ni Mkuu!”

17. Mimi ni maskini na fukara, ee Bwana;lakini ee Bwana wewe wanikumbuka.Ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu;uje, ee Mungu wangu, usikawie!