Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 42 Biblia Habari Njema (BHN)

KITABU CHA PILI

Sala ya MkimbiziZaburi 42 na 43 bila shaka zilikuwa wimbo mmoja hapo awali kama inavyoonekana dhahiri katika marudio ya aya ya 6 Zab 42 katika aya ya 11 na katika Zab 43 aya ya 5.

(Kwa Mwimbishaji. Utenzi wa Wakorahi)

1. Kama paa atamanivyo maji ya kijito,ndivyo ninavyokutamani, ee Mungu wangu!

2. Naona kiu ya Mungu, kiu ya Mungu aliye hai.Nitafika lini kwake na kuuona uso wake?

3. Machozi yamekuwa chakula changu mchana na usiku,waliponiambia kila siku: “Yuko wapi Mungu Wako!”

4. Nakumbuka tena mambo hayakwa majonzi moyoni mwangu:Jinsi nilivyokwenda na umati wa watu,nikawaongoza kwenda nyumbani kwa Munguwakipiga vigelegele vya shukrani;umati wa watu wakifanya sherehe!

5. Mbona nasononeka hivyo moyoni?Kwa nini nahangaika hivyo ndani mwangu?Nitamtumainia Mungu,maana nitamsifu tenayeye aliye msaada wangu na Mungu wangu.

6. Nimesongwa na huzuni moyoni mwangu,kwa hiyo ninakukumbuka wewe, ee Mungu,kutoka katika eneo la Yordani,kutoka mlima Hermoni na Mizari.

7. Nimeporomoshewa mafuriko ya majimafuriko ya maji yaja karibunayo yaita maporomoko mapya.Mawimbi na mapigo yako yamenikumba.

8. Mwenyezi-Mungu atanijalia fadhili zake mchana;nami nimwimbie wimbo wa sifa usiku,nimwombe Mungu anipaye uhai.

9. Namwambia Mungu, mwamba wangu:“Kwa nini umenisahau?Yanini niende huko na huko nikiombolezakwa kudhulumiwa na adui yangu?”

10. Nimepondwa kwa matukano yao,wanaponiuliza kila siku:“Yuko wapi, Mungu wako!”

11. Mbona nasononeka hivyo moyoni?Kwa nini nahangaika hivyo?Nitamtumainia Mungu,maana nitamsifu tena Mungu,aliye msaada wangu na Mungu wangu.