Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 22 Biblia Habari Njema (BHN)

Kilio

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo wa utenzi wa kulungu wa alfajiri. Zaburi ya Daudi)

1. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?Mbona uko mbali sana kunisaidia,mbali na maneno ya kilio changu?

2. Ee Mungu wangu, nalia mchana lakini hujibu;napiga yowe usiku, lakini nafuu sipati.

3. Hata hivyo, wewe ni mtakatifu;wewe watawala na kusifiwa na Waisraeli.

4. Wazee wetu walikutegemea;walikutegemea, nawe ukawaokoa.

5. Walikulilia wewe, wakaokolewa;walikutegemea, nao hawakuaibika.

6. Lakini mimi ni mdudu tu, wala si mtu;nimepuuzwa na kudharauliwa na watu.

7. Wote wanionao hunidhihaki;hunifyonya na kutikisa vichwa vyao.

8. Husema: “Alimtegemea Mwenyezi-Mungu,basi, Mungu na amkomboe!Kama Mungu anapendezwa naye,basi, na amwokoe!”

9. Lakini ndiwe uliyenitoa tumboni mwa mama yangu,uliniweka salama kifuani pa mama yangu.

10. Nimekutegemea tangu kuzaliwa kwangu.Tangu nilipozaliwa wewe umekuwa Mungu wangu.

11. Usikae mbali nami, kwani taabu imekaribia;wala hakuna wa kunisaidia.

12. Maadui wengi wanizunguka kama fahali;wamenisonga kama fahali wakali wa Bashani!

13. Wanafunua vinywa vyao kama simba,tayari kushambulia na kurarua.

14. Nimekwisha kama maji yaliyomwagika;mifupa yangu yote imeteguka;moyo wangu ni kama nta,unayeyuka ndani mwangu.

15. Koo langu limekauka kama kigae;ulimi wangu wanata kinywani mwangu.Umeniacha kwenye mavumbi ya kifo.

16. Genge la waovu limenizunguka;wananizingira kama kundi la mbwa;wamenitoboa mikono na miguu.

17. Nimebaki mifupa mitupu;maadui zangu waniangalia na kunisimanga.

18. Wanagawana nguo zangu,na kulipigia kura vazi langu.

19. Lakini wewe ee Mwenyezi-Mungu, usikae mbali nami;ewe msaada wangu, uje haraka kunisaidia.

20. Iokoe nafsi yangu mbali na upanga,yaokoe maisha yangu makuchani mwa mbwa hao!

21. Uniokoe kinywani mwa simba;iokoe nafsi yangu dhaifu toka pembe za nyati hao.

Wimbo wa shukrani

22. Nitawasimulia ndugu zangu matendo yako;nitakusifu kati ya kusanyiko lao:

23. Enyi mnaomcha Mwenyezi-Mungu, msifuni!Mtukuzeni enyi wazawa wote wa Yakobo!Mcheni Mungu enyi wazawa wote wa Israeli!

24. Maana yeye hapuuzi au kudharau unyonge wa mnyonge;wala hajifichi mbali naye,ila humsikia anapomwomba msaada.

25. Kwa sababu yako ninakusifukatika kusanyiko kubwa la watu;nitatimiza ahadi zangu mbele yao wakuchao.

26. Maskini watakula na kushiba;wanaomtafuta Mwenyezi-Mungu watamsifu.Mungu awajalie kuishi milele!

27. Ulimwengu wote utakumbuka na kumrudia Mwenyezi-Mungu;jamaa zote za mataifa zitamwabudu.

28. Maana Mwenyezi-Mungu ni mfalme;yeye anayatawala mataifa.

29. Wenye kiburi wote duniani watasujudu mbele yake;wote ambao hufa watainama mbele yake,wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.

30. Vizazi vijavyo vitamtumikia;watu watavisimulia habari za Mwenyezi-Mungu,

31. watatangaza matendo yake ya wokovu.Watu wasiozaliwa bado wataambiwa:“Mwenyezi-Mungu ndiye aliyefanya hayo!”