1. Ee Mwenyezi-Mungu, usinikemee kwa hasira yako;usiniadhibu kwa ghadhabu yako.
2. Unihurumie, ee Mwenyezi-Mungu, nimeishiwa nguvu;uniponye, ee Mwenyezi-Mungu, nataabika mpaka mifupani.
3. Ninahangaika sana rohoni mwangu.Ee Mwenyezi-Mungu, utakawia mpaka lini?
4. Unigeukie, ee Mwenyezi-Mungu, uniokoe;unisalimishe kwa sababu ya fadhili zako.
5. Huko kwa wafu hakuna anayekukumbuka;huko kuzimu ni nani awezaye kukusifu?
6. Niko hoi kwa kilio cha uchungu;kila usiku nalowesha kitanda changu kwa machozi;kwa kulia kwangu naulowesha mto wangu.
7. Macho yangu yamechoka kwa huzuni;yamefifia kwa kutaabishwa na adui.
8. Ondokeni kwangu enyi nyote watenda maovu!Maana Mwenyezi-Mungu amesikia kilio changu.
9. Mwenyezi-Mungu amesikia ombi langu;Mwenyezi-Mungu amekubali sala yangu.
10. Maadui zangu wote wataaibika na kufadhaika;watarudi nyuma na kuaibishwa ghafla.