Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 6 Biblia Habari Njema (BHN)

Sala wakati wa taabu

(Kwa Mwimbishaji: Na ala za nyuzi za muziki. Mtindo wa Sheminithi. Zaburi ya Daudi)

1. Ee Mwenyezi-Mungu, usinikemee kwa hasira yako;usiniadhibu kwa ghadhabu yako.

2. Unihurumie, ee Mwenyezi-Mungu, nimeishiwa nguvu;uniponye, ee Mwenyezi-Mungu, nataabika mpaka mifupani.

3. Ninahangaika sana rohoni mwangu.Ee Mwenyezi-Mungu, utakawia mpaka lini?

4. Unigeukie, ee Mwenyezi-Mungu, uniokoe;unisalimishe kwa sababu ya fadhili zako.

5. Huko kwa wafu hakuna anayekukumbuka;huko kuzimu ni nani awezaye kukusifu?

6. Niko hoi kwa kilio cha uchungu;kila usiku nalowesha kitanda changu kwa machozi;kwa kulia kwangu naulowesha mto wangu.

7. Macho yangu yamechoka kwa huzuni;yamefifia kwa kutaabishwa na adui.

8. Ondokeni kwangu enyi nyote watenda maovu!Maana Mwenyezi-Mungu amesikia kilio changu.

9. Mwenyezi-Mungu amesikia ombi langu;Mwenyezi-Mungu amekubali sala yangu.

10. Maadui zangu wote wataaibika na kufadhaika;watarudi nyuma na kuaibishwa ghafla.