Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 5 Biblia Habari Njema (BHN)

Sala wakati wa hatari

(Kwa Mwimbishaji: Na filimbi. Zaburi ya Daudi)

1. Usikilize maneno yangu, ee Mwenyezi-Mungu,usikie ninavyopiga kite.

2. Usikilize kilio changu,Mfalme wangu na Mungu wangu,maana wewe ndiwe nikuombaye.

3. Ee Mwenyezi-Mungu, alfajiri waisikia sauti yangu,asubuhi nakutolea tambiko yangu,kisha nangojea unijibu.

4. Wewe si Mungu apendaye ubaya;kwako uovu hauwezi kuwako.

5. Wenye majivuno hawastahimili mbele yako;wewe wawachukia wote watendao maovu.

6. Wawaangamiza wote wasemao uongo;wawachukia wauaji na wadanganyifu.

7. Lakini, kwa wingi wa fadhili zako,mimi nitaingia nyumbani mwako;nitakuabudu kuelekea hekalu lako takatifu,nitakusujudia kwa uchaji.

8. Uniongoze, ee Mwenyezi-Mungu, katika uadilifu wako,maana maadui zangu ni wengi;uiweke njia yako wazi mbele yangu.

9. Vinywani mwao hamna ukweli;mioyoni mwao wamejaa maangamizi,wasemacho ni udanganyifu wa kifo,ndimi zao zimejaa hila.

10. Uwaadhibu kwa hatia yao ee Mungu;waanguke kwa njama zao wenyewe;wafukuze nje kwa sababu ya dhambi zao nyingi,kwa sababu wamekuasi wewe.

11. Lakini wafurahi wote wanaokimbilia usalama kwako,waimbe kwa shangwe daima.Uwalinde wanaolipenda jina lako,wapate kushangilia kwa sababu yako.

12. Maana wewe Mwenyezi-Mungu wawabariki waadilifu;wawakinga kwa fadhili zako kama kwa ngao.