Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52

Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 8 Biblia Habari Njema (BHN)

1. “Wakati huo, nasema mimi Mwenyezi-Mungu, mifupa ya wafalme wa Yuda, mifupa ya wakuu wao, mifupa ya makuhani, mifupa ya manabii na mifupa ya wakazi wote wa Yerusalemu itachimbuliwa makaburini mwao.

2. Itaachwa imetandazwa mbele ya jua na mwezi na sayari zote za mbinguni, vitu ambavyo walivipenda na kuvitumikia, wakavitaka shauri na kuviabudu. Mifupa hiyo haitakusanywa wala kuzikwa, bali itakuwa kama mavi juu ya ardhi.

3. Watu wote waliobaki wa jamaa hii mbovu, mahali popote pale nilipowatawanya, wataona heri kufa kuliko kuishi. Ndivyo nisemavyo mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi.

Dhambi na adhabu

4. “Wewe Yeremia utawaambiakuwa mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi:Mtu akianguka, je hainuki tena?Mtu akipotea, je, hairudii tena njia yake?

5. Mbona basi, watu hawa wameacha njia iliyo sawana kuendelea katika upotovu wao?Wanashikilia miungu yao ya uongo,na kukataa kunirudia mimi!

6. Mimi nilisikiliza kwa makini,lakini wao hawakusema ukweli wowote.Hakuna mtu anayetubu uovu wake,wala kujiuliza; ‘Nimefanya nini?’Kila mmoja wao anashika njia yake,kama farasi akimbiliavyo moja kwa moja vitani.

7. Hata korongo anajua wakati wa kuhama;njiwa, mbayuwayu na koikoi,hufuata majira yao ya kurudi.Lakini watu wangu hawa hawajui kitujuu ya amri zangu mimi Mwenyezi-Mungu.

8. Mnawezaje kusema: ‘Sisi tuna hekima,sisi tunayo sheria ya Mwenyezi-Mungu,’hali waandishi wa sheria,wameipotosha sheria yangu?

9. Wenye hekima wenu wataaibishwa;watafadhaishwa na kunaswa.Wamelikataa neno la Mwenyezi-Mungu;je, ni hekima gani hiyo waliyo nayo?

10. Kwa hiyo, wake zao nitawapa watu wengine,mashamba yao nitawapa wengine.Maana, tangu mdogo hadi mkubwa,kila mmoja ana tamaa ya faida haramu.Tangu manabii hadi makuhani,kila mmoja anatenda kwa udanganyifu.

11. Wameliponya jeraha la watu wangu juujuu,wakisema, ‘Kuna amani, kuna amani’,kumbe hakuna amani yoyote!

12. Je, waliona aibu walipotenda machukizo hayo?La hasha! Hawakuona aibu hata kidogo.Hata hawajui kuona haya.Kwa hiyo, wataanguka pamoja na wale walioanguka;nitakapowaadhibu, wataangamia.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

13. “Mimi Mwenyezi-Mungu nasema:Nilipotaka kukusanya chochote kutoka kwao,sikupata zabibu hata moja juu ya mzabibu,sikupata tini zozote juu ya mtini;hata majani yao yamekauka.Hata nilichokuwa nimewapa kimetoweka.”

14. “Watu wanauliza: Kwa nini sisi tunakaa tu hapa?Kusanyikeni, tuingie katika miji yenye ngome,tukaangamie huko!Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, ametupangia tuangamie,ametupa maji yenye sumu tunywe,kwa kuwa tumemkosea yeye.

15. Tulitazamia kupata amani,lakini hakuna jema lililotokea.Tulitazamia wakati wa kuponywa,badala yake tukapata vitisho.

16. Sauti za farasi wao zinasikika,kwa mlio wa farasi wao wa vita,nchi nzima inatetemeka.Wanafika na kuiharibu nchi na vyote vilivyomo,kuangamiza mji pamoja na wote waishio humo.

(Mwenyezi-Mungu)

17. “Basi nitawaleteeni nyoka;nyoka wenye sumu wasioweza kurogwa na walozi,nao watawauma nyinyi.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

Huzuni ya Yeremia

18. Huzuni yangu haiwezi kutulizwa,moyo wangu wasononeka ndani yangu.

19. Sikiliza kilio cha watu wangu,kutoka kila upande katika nchi.“Je, Mwenyezi-Mungu hayuko Siyoni?Je, mfalme wake hayuko tena huko?”“Mbona wamenikasirisha kwa sanamu zao za miungu,na vinyago vyao vya miungu ya kigeni?”

(Mwenyezi-Mungu)

20. “Mavuno yamepita, kiangazi kimekwisha,nasi bado hatujaokolewa!

21. Jeraha la watu wangu limeniumiza moyoni,ninaomboleza na kufadhaika.

22. Je, hakuna dawa ya kupaka huko Gileadi?Je, hakuna mganga huko?Mbona basi watu wangu hawajaponywa?