Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52

Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 22 Biblia Habari Njema (BHN)

Ujumbe juu ya jumba la kifalme la Yuda

1. Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Nenda katika ikulu ya mfalme wa Yuda, uwape watu ujumbe huu:

2. Wewe mfalme wa Yuda unayekikalia kiti cha enzi cha mfalme Daudi, pamoja na watumishi wako na watu wako wanaopita katika malango haya, sikilizeni neno langu mimi Mwenyezi-Mungu.

3. Mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Tendeni mambo ya haki na uadilifu. Mwokoeni mikononi mwa mdhalimu mtu yeyote aliyenyanganywa mali zake. Msiwatendee vibaya au ukatili wageni, yatima na wajane wala msimwage damu ya mtu asiye na hatia mahali hapa.

4. Kama mkishika neno hili nililowaambia basi, wafalme wanaokikalia kiti cha enzi cha Daudi wataendelea kuingia kwa kupitia malango ya ikulu hii. Watapita pamoja na watumishi wao na watu wao, wakiwa wamepanda farasi na magari ya farasi.

5. Lakini kama hamtatii maneno haya, mimi Mwenyezi-Mungu naapa kwa nafsi yangu kwamba mahali hapa patakuwa magofu. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

6. Mwenyezi-Mungu asema hivi kuhusu ikulu ya mfalme wa Yuda:“Ingawa waonekana kuwa mzuri kama nchi ya Gileadikama kilele cha Lebanoni,Lakini naapa kuwa nitakufanya uwe jangwa,uwe mji usiokaliwa na watu.

7. Nitawatayarisha waangamizi dhidi yako,kila mmoja na silaha yake mkononi.Wataikata mierezi yako mizuri,na kuitumbukiza motoni.

8. “Kisha watu wengi wa mataifa watapita karibu na mji huu, na kila mmoja atamwuliza mwenzake: ‘Kwa nini Mwenyezi-Mungu ameutenda hivi mji huu mkubwa?’

9. Wenzao watawajibu, ‘Ni kwa sababu waliliacha agano la Mwenyezi-Mungu, Mungu wao, wakaiabudu miungu mingine na kuitumikia.’”

Ujumbe juu ya Shalumu

10. Msimlilie mtu aliyekufa,wala msiombolezee kifo chake.Bali mlilieni kwa uchungu yule aendaye mbali,kwa kuwa hatarudi tena kuiona nchi yake.

11. Maana, Mwenyezi-Mungu asema hivi juu ya Shalumu mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, aliyetawala baada ya Yosia baba yake, na ambaye aliondoka mahali hapa: “Shalumu hatarudi tena mahali hapa,

12. bali atafia hukohuko walikomchukua utumwani. Kamwe hataiona tena nchi hii.

Ujumbe juu ya Yehoyakimu

13. “Ole wako Yehoyakimuwewe unayejenga nyumba kwa dhulumana kuiwekea ghorofa bila kutumia haki.Unawaajiri watu wakutumikie burewala huwalipi mishahara yao.

14. Wewe wasema:‘Nitalijenga jumba kubwa,lenye vyumba vikubwa ghorofani.’Kisha huifanyia madirisha,ukafunika kuta zake kwa mbao za mierezi,na kuipaka rangi nyekundu!

15. Unadhani umekuwa mfalmekwa kushindana kujenga kwa mierezi?Baba yako alikula na kunywa,akatenda mambo ya haki na memandipo mambo yake yakamwendea vema.

16. Aliwapatia haki maskini na wahitaji,na mambo yake yakamwendea vema.Hii ndiyo maana ya kunijua mimi Mwenyezi-Mungu.

17. Lakini macho yako wewe na moyo wako,hungangania tu mapato yasiyo halali.Unamwaga damu ya wasio na hatia,na kuwatendea watu dhuluma na ukatili.

18. “Kwa hiyo, mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi juu ya Yehoyakimu mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda:Wakati atakapokufa,hakuna atakayemwombolezea akisema,‘Ole, kaka yangu!’‘Ole, dada yangu!’Hakuna atakayemlilia akisema,‘Maskini, bwana wangu!’‘Maskini, mfalme wangu!’

19. Atazikwa bila heshima kama punda,ataburutwa na kutupiliwa mbali,nje ya malango ya Yerusalemu.”

Maafa yatakayoipata Yerusalemu

20. Enyi watu wa Yerusalemu,pandeni Lebanoni mpige kelele,pazeni sauti zenu huko Bashani;lieni kutoka milima ya Abarimu,maana wapenzi wenu wote wameangamizwa.

21. Mwenyezi-Mungu aliongea nanyi mlipokuwa na fanaka,lakini nyinyi mkasema, “Hatutasikiliza.”Hii ndiyo tabia yenu tangu ujana wenu,hamjapata kuitii sauti ya Mwenyezi-Mungu.

22. Viongozi wenu watapeperushwa na upepo,wapenzi wenu watachukuliwa uhamishoni.Ndipo mtakapoona haya na kufadhaika,kwa sababu ya uovu wenu wote mliotenda.

23. Enyi wakazi wote wa Lebanoni,nyinyi mkaao salama kati ya mierezi;jinsi gani mtakavyopiga kite uchungu utakapowakumba,uchungu kama wa mama anayejifungua!

Hukumu ya Mungu juu ya Konia

24. Na kuhusu Konia mfalme wa Yuda, mwanawe Yehoyakimu, Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Naapa kwa nafsi yangu mimi Mwenyezi-Mungu kwamba hata kama wewe Konia mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, ungekuwa pete yangu ya mhuri katika mkono wangu wa kulia, ningekuvulia mbali.

25. Nitakutia mikononi mwa wale wanaotaka kuyamaliza maisha yako; naam, mikononi mwa wale unaowaogopa, mikononi mwa Nebukadneza, mfalme wa Babuloni; naam, mikononi mwa Wakaldayo.

26. Nitakufukuzia mbali katika nchi ya kigeni, wewe pamoja na mama yako mzazi. Mtakuwa watumwa katika nchi hiyo ambamo nyote wawili hamkuzaliwa, nanyi mtafia hukohuko.

27. Mtatamani kwa hamu kubwa kurudi katika nchi hii, lakini hamtarudi kamwe.

28. Je, huyu mtu Konia,amekuwa kama chungu kilichovunjika,ambacho hudharauliwa na kutupwa nje?Kwa nini yeye na watoto wake wametupwa mbaliwakatupwa katika nchi wasiyoijua?

29. Ee nchi, ee nchi, ee nchi!Sikia neno la Mwenyezi-Mungu!

30. Mwenyezi-Mungu asema hivi:Mwandike mtu huyu kwamba hana watoto,mtu ambaye hatafanikiwa maishani mwake.Maana hakuna hata mmoja wa wazawa wakeatakayekikalia kiti cha enzi cha Daudina kutawala tena katika Yuda.