Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52

Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 12 Biblia Habari Njema (BHN)

Yeremia anamhoji Mwenyezi-Mungu

1. Ee Mwenyezi-Mungu, wewe ni mwadilifu,ingawa nakulalamikia.Lakini ningependa kutoa hoja zangu mbele yako:Kwa nini waovu hufanikiwa katika mambo yao?Mbona wote wenye hila hustawi?

2. Unawaotesha nao wanaota;wanakua na kuzaa matunda.Wanakutaja kwa maneno yao,lakini mioyo yao iko mbali nawe.

3. Lakini wewe ee Mwenyezi-Mungu wanijua;wayathibiti maelekeo yangu kwako.Uwaokote hao kama kondoo wa kuchinjwa,watenge kwa ajili ya wakati wa kuuawa.

4. Mpaka lini nchi itaomboleza kwa ukame,na nyasi za mashamba yote kunyauka?Wanyama na ndege wanakufa kwa uovu wa wakazi wake;wanasema: “Mungu hataona mwisho wetu.”

5. Mwenyezi-Mungu asema,“Ikiwa umeshindana na waendao kwa miguu ukachoka,utawezaje kushindana na farasi?Kama unaanguka katika nchi isiyo na vizuizi,utafanyaje katika msitu wa Yordani?

6. Hata ndugu zako, jamaa yako mwenyewe,nao pia wamekutendea mambo ya hila;wanakukemea waziwazi.Usiwaamini hata kidogo,japo wanakuambia maneno mazuri.”

Mungu anaiacha nyumba yake na watu wake

7. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Nimeiacha nyumba yangu;nimeitupa mali yangu mimi mwenyewe.Israeli, mpenzi wangu wa moyo,nimemtia mikononi mwa maadui zake.

8. Wateule wangu wamenigeuka,wamekuwa kama simba porini,wameningurumia mimi;ndiyo maana nawachukia.

9. Wateule wangu wamekuwa ndege mzuriwanaoshambuliwa na kozi pande zote.Nenda ukawakusanye wanyama wote wakaliwaje kushiriki katika karamu.

10. Wachungaji wengi wameharibu shamba langu la mizabibu,wamelikanyagakanyaga chini lililo mali yangu;shamba langu zuri wamelifanya jangwa.

11. Wamelifanya kuwa tupu;katika ukiwa wake lanililia.Nchi yote imekuwa jangwa,wala hakuna mtu anayejali.

12. Juu ya milima yote jangwani,watu wamefika kuangamiza.Upanga wangu unapita kuiangamiza nchi,toka upande mmoja hadi mwingine,wala hakuna mtu atakayeishi kwa amani.

13. Walipanda ngano, lakini walivuna magugu;walifanya bidii, lakini hawakupata kitu.Kwa sababu ya hasira yangu kali,mavuno watakayoyapata yatakuwa aibu tupu.”

Mungu na majirani wa Israeli

14. Mwenyezi-Mungu asema hivi juu ya jirani wabaya wa watu wangu: “Wamekigusa kile kilicho changu, kile nilichowapa watu wangu Israeli! Basi nitawangoa kutoka katika nchi yao. Hata watu wa Yuda nitawangoa katika nchi yao.

15. Lakini baada ya kuwangoa, nitawahurumia tena; nitalirudisha kila taifa katika sehemu yake na katika nchi yake.

16. Na kama watajifunza njia za watu wangu kwa moyo wote, kama wataapa kwa jina langu kwa kusema, ‘Kama aishivyo Mwenyezi-Mungu,’ kama vile walivyowafundisha watu wangu kuapa kwa jina la mungu Baali, basi watajengeka miongoni mwa watu wangu.

17. Lakini taifa lolote ambalo halitanitii, nitalingoa kabisa na kuliangamiza. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”