Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52

Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 13 Biblia Habari Njema (BHN)

Kikoi cha kitani

1. Mwenyezi-Mungu aliniambia hivi: “Nenda ukajinunulie kikoi cha kitani, ukajifunge kiunoni; lakini usikitie majini.”

2. Basi, nikaenda, nikanunua kikoi kama alivyoniagiza Mwenyezi-Mungu, nikajifunga kiunoni.

3. Kisha, neno la Mwenyezi-Mungu likanijia mara ya pili:

4. “Kichukue kikoi ulichonunua na ambacho umejifunga kiunoni, uende kwenye mto Eufrate na kukificha katika pango mwambani.”

5. Basi, nikaenda na kukificha kikoi hicho karibu na mto Eufrate, kama Mwenyezi-Mungu alivyoniamuru.

6. Ikawa, baada ya siku nyingi, Mwenyezi-Mungu akaniambia, “Nenda kwenye mto Eufrate, ukakichukue kile kikoi nilichokuamuru ukifiche huko.”

7. Basi, nikaenda kwenye mto Eufrate, nikachimbua na kukitoa kile kikoi mahali nilipokuwa nimekificha. Nilipokitoa, nilishangaa kukiona kuwa kilikuwa kimeharibika kabisa; kilikuwa hakifai tena.

8. Ndipo neno la Mwenyezi-Mungu likanijia:

9. “Mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Hivi ndivyo nitakavyokiharibu kiburi cha Yuda na kiburi kikubwa cha Yerusalemu.

10. Watu hawa waovu wanakataa kusikia maneno yangu, na badala yake wanakuwa wakaidi na kufuata mawazo yao wenyewe. Wanaifuata miungu mingine, wanaitumikia na kuiabudu. Hao watakuwa kama kikoi hiki ambacho hakifai kitu.

11. Kama vile kikoi kinavyoshikamana na kiuno cha mtu, ndivyo nilivyowashikamanisha nami watu wa Israeli na watu wa Yuda, ili wajulikane kwa jina langu, wanisifu na kunitukuza. Lakini wao hawakunisikiliza. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

Mtungi wa divai na hasira ya Mungu

12. Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli, aliniambia hivi: “Waambie watu wa Israeli kwamba kila mtungi utajazwa divai. Lakini utakapowaambia hivyo, wao watakujibu hivi: ‘Kwani unadhani sisi hatujui kwamba kila mtungi utajazwa divai?’

13. Nawe utawaambia kuwa mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Nitawalewesha wenyeji wote wa nchi hii; wafalme wanaotawala mahali pa Daudi, makuhani, manabii na wakazi wote wa Yerusalemu.

14. Nitawagonganisha wao kwa wao kina baba na watoto. Sitawahurumia, sitawaachia wala sitawarehemu, bali nitawaangamiza.”

Yeremia anaonya juu ya majivuno

15. Enyi Waisraeli, sikilizeni kwa makini,msiwe na majivuno maana Mwenyezi-Mungu anasema nanyi.

16. Mtukuzeni Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu,kabla hajawaletea giza,nanyi mkajikwaa miguu kwenye milima ya giza.Nyinyi mnatazamia mwanga,lakini anaugeuza kuwa utusitusina kuufanya kuwa giza nene.

17. Lakini kama msiponisikiliza,moyo wangu utalia machozi faraghani,kwa sababu ya kiburi chenu.Nitalia kwa uchungu na kububujika machozi,kwa kuwa watu wa Mwenyezi-Mungu wametekwa.

Ujumbe wa Mungu kwa jamii ya kifalme

18. Mwambie mfalme na mama yake hivi:“Shukeni kwenye viti vyenu vya enzi,maana taji zenu nzuri zimeanguka vichwani mwenu.

19. Miji ya Negebu imezingirwa;hakuna awezaye kufungua malango yake.Watu wa Yuda wamechukuliwa mateka,wote kabisa wamepelekwa utumwani.”

20. Inua macho yako, ee Yerusalemu!Tazama! Madui zako waja kutoka kaskazini.Kundi ulilokabidhiwa liko wapi?Kundi lako zuri li wapi?

21. Utasemaje juu ya wale uliodhani ni rafiki,wale ambao wewe mwenyewe uliwafundisha,watakapokushinda na kukutawala?Je, si utakumbwa na uchungukama wa mama anayejifungua?

22. Nawe utajiuliza moyoni mwako,“Kwa nini mambo haya yamenipata?”Sawa! Kama vazi lako limepandishwa juu,nawe ukatendewa kwa ukatili mno,hayo ni matokeo ya makosa yako mengi mno.

23. Je, Mwethiopia aweza kubadili rangi yake,au chui madoadoa yake?Ikiwezekana, nanyi pia mnaweza kutenda mema,nyinyi mliozoea kutenda maovu!

24. Mwenyezi-Mungu atawatawanya kama makapiyanayopeperushwa na upepo kutoka jangwani.

25. Mwenyezi-Mungu asema:“Hayo ndiyo yatakayokupata,ndivyo nilivyoamua kukutenda mimi Mwenyezi-Mungu,kwa sababu umenisahau mimi,ukaamini miungu ya uongo.

26. Nitalipandisha vazi lako hadi kichwanina aibu yako yote itaonekana wazi.

27. Nimeyaona machukizo yako:Naam, uzinifu wako na uzembe wako,na uasherati wako wa kupindukia,juu ya milima na mashambani.Ole wako ee Yerusalemu!Mpaka lini utakaa bila kutakaswa?”