Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52

Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 10 Biblia Habari Njema (BHN)

Ibada za sanamu na ibada za kweli

1. Sikilizeni neno analowaambieni Mwenyezi-Mungu,enyi Waisraeli!

2. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Msijifunze mienendo ya mataifa mengine,wala msishangazwe na ishara za mbinguni;yaacheni mataifa mengine yashangazwe nazo.

3. Maana, mila za dini za watu hawa ni za uongo.Mtu hukata mti msitunifundi akachonga kinyago cha mungu kwa shoka.

4. Kisha watu hukipamba kwa fedha na dhahabuwakakipigilia misumari kwa nyundoili kisije kikaanguka.

5. Vinyago vyao ni kama vinyago vya kutishia ndegekatika shamba la matango,havina uwezo wa kuongea;ni lazima vibebwemaana haviwezi kutembea.Msiviogope vinyago hivyo,maana haviwezi kudhuru,wala haviwezi kutenda lolote jema.”

6. Ee Mwenyezi-Mungu, hakuna aliye kama wewe;wewe ni mkuu na nguvu yako yajulikana.

7. Nani asiyekuogopa wewe, ee mfalme wa mataifa?Wewe wastahili kuheshimiwa.Miongoni mwa wenye hekima wote wa mataifa,na katika falme zao zote,hakuna hata mmoja aliye kama wewe.

8. Wote ni wajinga na wapumbavumafunzo ya vinyago ni upuuzi mtupu!

9. Vinyago hivyo hupambwa kwa fedha kutoka Tarshishi,na dhahabu kutoka Ofiri;kazi ya mafundi stadi na wafua dhahabu.Zimevishwa nguo za samawati na zambarau,zilizofumwa na wafumaji stadi.

10. Lakini Mwenyezi-Mungu ni Mungu wa kweli;Mungu aliye hai, mfalme wa milele.Akikasirika, dunia hutetemeka,mataifa hayawezi kustahimili hasira yake.

11. Basi, utawaambia hivi: “Miungu ambayo haikuumba mbingu na dunia, itaangamia. Itatoweka kabisa duniani na chini ya mbingu.”

Wimbo wa kumsifu Mungu

12. Mwenyezi-Mungu aliiumba dunia kwa nguvu zake;kwa hekima yake aliuimarisha ulimwengu,kwa akili yake alizitandaza mbingu.

13. Anapotoa sauti yake, maji hunguruma mbinguni,huzusha ukungu kutoka mipaka ya dunia.Huufanya umeme umulike wakati wa mvua,na kuutoa upepo katika ghala zake.

14. Binadamu ni mjinga na mpumbavu;kila mfua dhahabu huaibishwa na vinyago vyake;maana, vinyago hivyo ni uongo mtupu.Havina uhai wowote ndani yao.

15. Havina thamani, ni udanganyifu mtupu;wakati vitakapoadhibiwa vyote vitaangamia.

16. Lakini Mungu wa Yakobo si kama vinyago hivyo,maana, yeye ndiye aliyeumba vitu vyote,na Israeli ni taifa lililo mali yake;Mwenyezi-Mungu wa majeshi ndilo jina lake.

Uhamisho unakaribia

17. Kusanyeni vitu vyenu enyi watu mliozingirwa.

18. Maana Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Wakati huo nitawatupa nje ya nchi hii,nitawataabisha asibaki mtu yeyote.”

19. Ole wangu mimi Yerusalemu maana nimejeruhiwa!Jeraha langu ni baya sana!Lakini nilisema: “Hakika haya ni mateso,na sina budi kuyavumilia.”

20. Lakini hema langu limebomolewa,kamba zake zote zimekatika;watoto wangu wameniacha, na kwenda zao,wala hawapo tena;hakuna wa kunisimikia tena hema langu,wala wa kunitundikia mapazia yangu.

21. Nami Yeremia nikasema:Wachungaji wamekuwa wajinga,hawakuomba shauri kwa Mwenyezi-Mungu;kwa sababu hiyo, hawakufanikiwa,na kondoo wao wote wametawanyika.

22. Sikilizeni sauti! Habari zinatufikia.Kuna kishindo kutoka kaskazini.Taifa kutoka kaskazini linakuja,kuifanya miji ya Yuda kuwa jangwaambamo kutakuwa na mapango ya mbweha!

23. Najua, ee Mwenyezi-Mungu,binadamu hana uwezo na maisha yake;hakuna mtu awezaye kuyaongoza maisha yake.

24. Utukosoe, ee Mwenyezi-Mungu, lakini si kwa ghadhabu,wala kwa hasira yako, tusije tukaangamia.

25. Imwage hasira yako juu ya mataifa yasiyokuabudu,na juu ya watu ambao hawakutambui.Maana, wamewaua wazawa wa Yakobo;wamewaua na kuwaangamiza kabisa,na nchi yao wameiacha magofu.