Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52

Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 47 Biblia Habari Njema (BHN)

Tamko la Mwenyezi-Mungu juu ya Filistia

1. Neno la Mwenyezi-Mungu lililomjia nabii Yeremia kuhusu Wafilisti, kabla Farao hajaushambulia mji wa Gaza:

2. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Tazama! Maji yanapanda kutoka kaskazini,nayo yatakuwa mto uliofurika;yataifunika nchi nzima na vyote vilivyomo,mji na wakazi na wanaoishi humo.Watu watalia,wakazi wote wa nchi wataomboleza.

3. Watasikia mshindo wa kwato za farasi,kelele za magari ya vita,na vishindo vya magurudumu yao.Kina baba watawasahau watoto wao,mikono yao itakuwa imelegea mno.

4. Hiyo ni siku ya kuwaangamiza Wafilisti wote,kukomesha msaada uliobakia kutoka Tiro na Sidoni.Maana Mwenyezi-Mungu anawaangamiza Wafilisti,watu waliosalia wa kisiwa cha Kaftori.

5. Watu wa Gaza wamenyoa upara kuomboleza;mji wa Ashkeloni umeangamia.Enyi watu wa Anakimu mliobakimpaka lini mtajikatakata kwa huzuni?

6. Ee upanga wa Mwenyezi-Mungu!Utachukua muda gani ndipo utulie?Ingia katika ala yako,ukatulie na kunyamaa!

7. Lakini utawezaje kutulia,hali Mwenyezi-Mungu ameupa kazi?Ameuamuru ushambulie mji wa Ashkelonina watu wanaoishi pwani.”