Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52

Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 4 Biblia Habari Njema (BHN)

Wito wa toba

1. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Ukitaka kurudi ee Israeli, nirudie mimi.Ukiviondoa vitu vya kuchukiza mbele yangu,usipotangatanga huko na huko,

2. ukiapa kwa ukweli, unyofu na uadilifu,kwa kusema, ‘Kama Mwenyezi-Mungu aishivyo’,ndipo mataifa yatakapopata baraka kwangu,na kutukuka kwa sababu yangu.”

3. Mwenyezi-Mungu awaambia hivi watu wa Yuda na wakazi wa Yerusalemu:“Limeni mashamba yenu mapya;msipande mbegu zenu penye miiba.

4. Enyi watu wa Yuda na wakazi wa Yerusalemu,jitakaseni kwa ajili yangu mimi Mwenyezi-Mungu,wekeni mioyo yenu wazi mbele yangu.La sivyo, ghadhabu yangu itachomoza kama moto,iwake hata pasiwe na mtu wa kuizima,kwa sababu ya uovu wa matendo yenu.

Yuda hatarini

5. “Tangazeni huko Yuda,pazeni sauti huko Yerusalemu!Pigeni tarumbeta kila mahali nchini!Pazeni sauti na kusema:Kusanyikeni pamoja!Kimbilieni miji yenye ngome!

6. Twekeni bendera ya vita kuelekea Siyoni,kimbilieni usalama wenu, msisitesite!Mwenyezi-Mungu analeta maafana maangamizi makubwa kutoka kaskazini.

7. Kama simba atokavyo mafichoni mwake,mwangamizi wa mataifa ameanza kuja,anakuja kutoka mahali pake,ili kuiharibu nchi yako.Miji yako itakuwa magofu matupu,bila kukaliwa na mtu yeyote.

8. Kwa hiyo, vaa vazi la gunia,omboleza na kulia;maana, hasira kali ya Mwenyezi-Mungu,bado haijaondoka kwetu.

9. Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Siku hiyo, mfalme na wakuu watakufa moyo; makuhani watapigwa na bumbuazi, na manabii watashangaa.”

10. Kisha nikasema: “Aa, Mwenyezi-Mungu, hakika umewadanganya kabisa watu hawa na mji wa Yerusalemu! Uliwaambia mambo yatawaendea vema, kumbe maisha yao yamo hatarini kabisa!”

11. Wakati huo, wataambiwa hivi watu hawa pamoja na mji wa Yerusalemu, “Upepo wa hari kutoka vilele vikavu vya jangwani utawavumia watu wangu. Huo si upepo wa kupepeta au kusafisha,

12. bali ni upepo mkali sana utokao kwangu. Ni mimi Mwenyezi-Mungu nitakayetoa hukumu juu yao.”

Yuda imezingirwa na maadui

13. Tazama! Adui anakuja kama mawingu.Magari yake ya vita ni kama kimbunga,na farasi wake waenda kasi kuliko tai.Ole wetu! Tumeangamia!

14. Yerusalemu, yasafishe maovu moyoni mwako,ili upate kuokolewa.Mpaka lini utaendelea kuwaza maovu?

15. Sauti kutoka Dani inatoa taarifa;inatangaza maafa kutoka vilima vya Efraimu.

16. Inayaonya mataifa,inaitangazia Yerusalemu:“Wavamizi waja kutoka nchi ya mbali,wanaitisha miji ya Yuda,

17. wanauzingira Yerusalemu kama walinda mashamba,kwa sababu watu wake wameniasi mimi Mwenyezi-Mungu.

18. Yuda, mwenendo wako na matendo yako yamekuletea hayo.Hayo ndiyo maafa yaliyokupata, tena ni machungu;yamepenya mpaka ndani moyoni mwako.”

Yeremia awasikitikia watu wake

19. Uchungu, uchungu!Nagaagaa kwa uchungu!Moyo wangu unanigonga vibaya.Wala siwezi kukaa kimya.Maana naogopa mlio wa tarumbeta,nasikia kingora cha vita.

20. Maafa baada ya maafa,nchi yote imeharibiwa.Ghafla makazi yangu yameharibiwa,na hata mapazia yake kwa dakika moja.

21. Hadi lini nitaona bendera ya vitana kuisikia sauti ya tarumbeta?

22. Mwenyezi-Mungu asema:“Watu wangu ni wapumbavu,hawanijui mimi.Wao ni watoto wajinga;hawaelewi kitu chochote.Ni mabingwa sana wa kutenda maovu,wala hawajui kutenda mema.”

Ono la Yeremia kuhusu maangamizi

23. Niliiangalia nchi, lo! Imekuwa mahame na tupu;nilizitazama mbingu, nazo hazikuwa na mwanga.

24. Niliiangalia milima, lo, ilikuwa inatetemeka,na vilima vyote vilikuwa vinayumbayumba.

25. Nilikodoa macho wala sikuona mtu;hata ndege angani walikuwa wametoweka.

26. Niliona nchi yenye rutuba imekuwa jangwa,na miji yake yote imekuwa magofu matupu,kwa sababu ya hasira kali ya Mwenyezi-Mungu.

27. Maana Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Nchi nzima itakuwa jangwa tupu;lakini sitaiharibu kabisa.

28. Kwa hiyo, nchi itaomboleza,na mbingu zitakuwa nyeusi.Maana, nimetamka na sitabadili nia yangu;nimeamua, wala sitarudi nyuma.

29. Watakaposikika wapandafarasi na wapiga mishale,kila mmoja atatimua mbio.Baadhi yao watakimbilia msituni,wengine watapanda majabali.Kila mji utaachwa tupu;hakuna mtu atakayekaa ndani.

30. Nawe Yerusalemu uliyeachwa tupu,unavalia nini mavazi mekundu?Ya nini kujipamba kwa dhahabu,na kujipaka wanja machoni?Unajirembesha bure!Wapenzi wako wanakudharau sana;wanachotafuta ni kukuua.

31. Nilisikia sauti kama ya mwanamke anayejifungua,yowe kama anayejifungua mtoto wa kwanza.Ilikuwa sauti ya Yerusalemu akitweta,na kuinyosha mikono yake akisema,‘Ole wangu!Wanakuja kuniua!’”