Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52
  53. 53
  54. 54
  55. 55
  56. 56
  57. 57
  58. 58
  59. 59
  60. 60
  61. 61
  62. 62
  63. 63
  64. 64
  65. 65
  66. 66

Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 46 Biblia Habari Njema (BHN)

1. “Wewe Beli umeanguka;Nebo umeporomoka.Wakati mmoja watu walibeba sanamu zenu.Sasa wanazibeba mgongoni mwa wanyama,hao wanyama wachovu wamelemewa.

2. Nyinyi mmeanguka na kuvunjika,hamwezi kuviokoa vinyago vyenu;nyinyi wenyewe pia mtapelekwa uhamishoni!

3. “Sikilizeni enyi wazawa wa Yakobo,nisikilizeni enyi mabaki ya watu wangu wa Israeli.Mimi niliwatunzeni tangu mlipozaliwa;niliwabebeni tangu tumboni mwa mama yenu.

4. Mimi ni yuleyule hata katika uzee wenu;hata katika uzee wenu mimi nitawabeba.Nilifanya hivyo kwanza,nitafanya hivyo tena.Nitawabeba nyinyi na kuwaokoa.

5. “Mtanifananisha na nani, tufanane?Je, mwaweza kunilinganisha na nani, tulingane?

6. Watu humimina dhahabu kutoka mifuko yao,hupima fedha kwenye mizani zao,wakamwajiri mfua dhahabu atengeneze sanamukisha huisujudu na kuiabudu!

7. Hujitwisha sanamu hiyo mabegani, wakaibeba,kisha huiweka mahali pake, ikakaa papo hapo;kamwe haiwezi hata kusogea kutoka hapo ilipo.Mtu akiililia, haiwezi kumwitikia,wala haiwezi kumwokoa mtu katika taabu zake.

8. “Kumbukeni jambo hili na kutafakari,liwazeni akilini mwenu enyi wakosefu.

9. Kumbukeni mambo niliyotenda hapo kale!Mimi ndimi Mungu na hakuna mwingine;naam, mimi ni Mungu, wala hakuna mwingine kama mimi.

10. Nilitangaza mambo ya mwisho tangu mwanzo,tangu kale nilitangaza mambo yatakayotukia.Lengo langu litatimia;mimi nitatekeleza nia yangu yote.

11. Ninamwita tai wangu kutoka mashariki,naam, msiri wangu kutoka nchi ya mbali.Mimi nimenena na nitayafanya;mimi nimepanga nami nitatekeleza.

12. “Nisikilizeni, enyi wenye vichwa vigumu,nisikilizeni enyi mlio mbali na ukombozi.

13. Siku ya kuwakomboa naileta karibu,haiko mbali tena;siku ya kuwaokoeni haitachelewa.Nitauokoa mji wa Siyoni,kwa ajili ya Israeli, fahari yangu.