Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52
  53. 53
  54. 54
  55. 55
  56. 56
  57. 57
  58. 58
  59. 59
  60. 60
  61. 61
  62. 62
  63. 63
  64. 64
  65. 65
  66. 66

Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 24 Biblia Habari Njema (BHN)

Mwenyezi-Mungu ataiadhibu dunia

1. Sasa Mwenyezi-Mungu anaiharibu duniana kuifanya tupu.Atausokota uso wa duniana kuwatawanya wakazi wake.

2. Kila mtu atapatwa na mambo yaleyale:Mtu wa kawaida na kuhani;mtumwa na bwana wake;mjakazi na bibi yake;mnunuzi na mwuzaji;mkopeshaji na mkopaji;mdai na mdaiwa.

3. Dunia itaharibiwa kabisa na kuangamizwa;Mwenyezi-Mungu ametamka hayo.

4. Dunia inakauka na kunyauka;ulimwengu unafadhaika na kunyauka;mbingu zinafadhaika pamoja na dunia.

5. Watu wameitia najisi duniamaana wamezivunja sheria za Mungu,wamezikiuka kanuni zake,wamelivunja agano lake la milele.

6. Kwa sababu hiyo laana inaitokomeza dunia,wakazi wake wanateseka kwa makosa yao.Wakazi wa dunia wamepungua,ni watu wachache tu waliosalia.

7. Mizabibu inanyauka,divai inakosekana.Wote waliokuwa wenye furahasasa wanasononeka kwa huzuni.

8. Mdundo wa vigoma umekoma,nderemo na vifijo vimetoweka;midundo ya vinubi imekomeshwa.

9. Hakuna tena kunywa divai na kuimba;mvinyo umekuwa mchungu kwa wanywaji.

10. Mji uliohamwa umejaa uharibifu;kila nyumba imefungwa asiingie mtu.

11. Kuna kilio barabarani kwa kukosa divai;shangwe yote imekoma,furaha imetoweka duniani.

12. Mji ni magofu matupu;malango yake yamevunjwavunjwa.

13. Kama vile zeituni chache tu juu ya mzeituniau tini chache tu juu ya mtinibaada ya kumaliza mavuno,ndivyo itakavyokuwa katika nchi zote:Watu wachache watabakia hai.

14. Watakaosalia watapaza sauti,wataimba kwa shangwe.Kutoka magharibi watatangaza ukuu wa Mwenyezi-Mungu,

15. nao wakazi wa mashariki watamsifu.Watu wa mbali watalisifujina la Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli.

16. Tunasikia nyimbo za sifa kutoka miisho ya dunia,nyimbo za kumsifu Mungu aliye mwadilifu.Lakini mimi ninanyongonyea,naam, ninanyongonyea.Ole wangu mimi!Wasaliti wanaendelea kuwa wasaliti,usaliti wao unazidi kuwa mbaya zaidi.

17. Hofu, mashimo na mitego,hivi ndivyo vinavyowangojeni enyi wakazi wa dunia.

18. Atakayeikimbia hofu atatumbukia shimoni;atakayetoka shimoni atanaswa mtegoni.Madirisha ya mbinguni yamefunguliwa,misingi ya dunia inatikisika.

19. Dunia inavunjikavunjika,inapasuka na kutikiswatikiswa.

20. Inapepesuka kama mlevi,inayumbayumba kama kibanda.Imelemewa na mzigo wa dhambi zakenayo itaanguka wala haitainuka tena.

21. Siku ile Mwenyezi-Mungu ataliadhibu jeshi la anganikadhalika na wafalme wa duniani.

22. Wote watakusanywa kama wafungwa shimoni;watafungwa gerezani pamoja kwa miaka mingi,na baada ya muda huo atawaadhibu.

23. Kisha mwezi utaaibishwa,nalo jua litaona aibu kuangaza,kwa kuwa Mwenyezi-Mungu wa majeshiatatawala huko Yerusalemu katika mlima Siyoni;ataonesha wazee wa watu wake utukufu wake.