Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52
  53. 53
  54. 54
  55. 55
  56. 56
  57. 57
  58. 58
  59. 59
  60. 60
  61. 61
  62. 62
  63. 63
  64. 64
  65. 65
  66. 66

Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 55 Biblia Habari Njema (BHN)

Njoni hata kama hamna fedha

1. “Haya! Kila mwenye kiu na aje kwenye maji!Njoni, nyote hata msio na fedha;nunueni ngano mkale,nunueni divai na maziwa.Bila fedha, bila gharama!

2. Mbona mnatumia fedha yenukwa ajili ya kitu kisicho chakula?Ya nini kutoa jasho lenu kwa kitu kisichoshibisha?Nisikilizeni mimi kwa makini,nanyi mtakula vilivyo bora,na kufurahia vinono.

3. “Tegeni sikio enyi watu wangu, mje kwangu;nisikilizeni, ili mpate kuishi.Nami nitafanya nanyi agano la milele;nitawapeni fadhili nilizomwahidi Daudi.

4. Mimi nilimfanya kiongozi na kamanda wa mataifaili yeye anishuhudie kwa watu wa mataifa.

5. Sasa utayaita mataifa usiyoyajua,watu wa mataifa yasiyokutambua watakujia mbio,kwa sababu yangu mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako;kwa sababu yangu mimi Mtakatifu wa Israeliniliyekufanya wewe utukuke.”

6. Mtafuteni Mwenyezi-Mungu wakati bado anapatikana,mwombeni msaada wakati yupo bado karibu.

7. Waovu na waache njia zao mbaya,watu wabaya waachane na mawazo yao mabaya;wamrudie Mwenyezi-Mungu apate kuwahurumia,wamwendee Mungu wetu maana atawasamehe.

8. Maana, Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Mawazo yangu si kama mawazo yenu,wala njia zangu si kama njia zenu.

9. Kama vile mbingu zilivyo mbali na dunia,ndivyo njia zangu zilivyo mbali na zenu,na mawazo yangu mbali na mawazo yenu.

10. “Kama vile mvua na theluji ishukavyo toka mbinguni,wala hairudi huko bali huinywesha ardhi,ikaifanya ichipue mimea ikakua,ikampatia mpanzi mbegu na kuwapa watu chakula,

11. vivyo hivyo na neno langu mimi:Halitanirudia bila mafanikio,bali litatekeleza matakwa yangu,litafanikiwa lengo nililoliwekea.

12. “Mtatoka Babuloni kwa furaha;mtaongozwa mwende kwa amani.Milima na vilima mbele yenu vitapaza sauti na kuimba,na miti yote mashambani itawapigia makofi.

13. Badala ya michongoma kutamea misonobari,na badala ya mbigili kutamea mihadasi.Hilo litakuwa jambo litakalowakumbusha watujuu ya mambo niliyotenda mimi Mwenyezi-Mungu;ishara ya milele ambayo haitafutwa.”