Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52
  53. 53
  54. 54
  55. 55
  56. 56
  57. 57
  58. 58
  59. 59
  60. 60
  61. 61
  62. 62
  63. 63
  64. 64
  65. 65
  66. 66

Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 11 Biblia Habari Njema (BHN)

Ufalme wa amani

1. Kutatokea chipukizi katika kisiki cha Yese,tawi litachipua mizizini mwake.

2. Roho ya Mwenyezi-Mungu itakaa kwake,roho ya hekima na maarifa,roho ya shauri jema na nguvu,roho ya ujuzi na ya kumcha Mwenyezi-Mungu.

3. Atafurahia kumcha Mwenyezi-Mungu.Hatahukumu kadiri ya mambo ya njenje,wala kuamua kufuatana na yale anayosikia.

4. Atawapatia haki watu maskini,atawaamulia sawasawa wanyonge nchini.Kwa neno lake ataiadhibu dunia,kwa tamko lake atawaua waovu.

5. Haki itakuwa kama mkanda wa kujifunga,uaminifu utakaa naye kama mkanda kiunoni.

6. Mbwamwitu ataishi pamoja na mwanakondoo,chui watapumzika pamoja na mwanambuzi.Ndama na wanasimba watakula pamoja,na mtoto mdogo atawaongoza.

7. Ngombe na dubu watakula pamoja,ndama wao watapumzika pamoja;na simba atakula majani kama ng'ombe.

8. Mtoto mchanga atacheza kwenye shimo la nyokamtoto ataweza kutia mkono shimoni mwa nyoka wa sumu.

9. Katika mlima mtakatifu wa Munguhakutakuwa na madhara wala uharibifu.Maana kumjua Mwenyezi-Mungu kutaenea pote nchini,kama vile maji yajaavyo baharini.

Walio uhamishoni watarudi

10. Siku ile chipukizi wa Yese atakuwa ishara kwa mataifa; mataifa yatamtafuta na makazi yake yatatukuka.

11. Siku hiyo, Bwana ataunyosha mkono wake tena kuwarejesha watu wake waliosalia huko Ashuru, Misri, Pathrosi, Kushi, Elamu, Shinari, Hamathi na sehemu za pwani.

12. Naye atatweka bendera kuwaashiria mataifa,kuwakusanya Waisraeli waliodharauliwa,kuwaleta pamoja watu wa Yuda waliotawanywa,na kuwarudisha toka pembe nne za dunia.

13. Wivu wa Efraimu juu ya Yuda utakoma,hakutakuwa tena na uadui kati ya Yuda na Efraimu.

14. Wote pamoja watawavamia Wafilisti walio magharibi,pamoja watawapora watu wakaao mashariki.Watawashinda Waedomu na Wamoabu,nao Waamoni watawatii.

15. Mwenyezi-Mungu atakausha ghuba ya bahari ya Shamu,kwa pumzi yake ichomayo atakausha mto Eufrate,nao utagawanyika katika vijito saba,watu wavuke humo miguu mikavu.

16. Tena, kutakuwa na barabara kuu toka Ashurukwa ajili ya watu wake waliobaki humokama ilivyokuwa kwa Waisraeliwakati walipotoka nchini Misri.