Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52
  53. 53
  54. 54
  55. 55
  56. 56
  57. 57
  58. 58
  59. 59
  60. 60
  61. 61
  62. 62
  63. 63
  64. 64
  65. 65
  66. 66

Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 15 Biblia Habari Njema (BHN)

Mungu ataiangamiza Moabu

1. Kauli ya Mungu dhidi ya nchi ya Moabu.Mji wa Ari nchini Moabu umeangamizwa usiku;mji wa Kiri nchini Moabu umeteketezwa usiku.

2. Watu wa Diboni wamepanda hekaluni, hadi mahali pa juu kuomboleza,watu wa Moabu wanalia kwa ajili ya Nebo na Medeba;vichwa vyote vimenyolewa upara,ndevu zao zote zimekatwa kabisa.

3. Wanapita njiani wamevaa mavazi ya gunia.Kwenye paa za nyumba na viwanja vya mjiwatu wanalia na kukauka kwa machozi.

4. Watu wa Heshboni na Eleale wanalia,sauti zao zinasikika hadi Yahazi.Hata askari wa Moabu wanalia kwa sauti;mioyo yao inatetemeka.

5. Moyo wangu unasononeka juu ya nchi ya Moabu;wakimbizi wake wanakimbilia Soari,wanakimbia mpaka Eglath-shelishiya.Wanapanda njia ya kwenda Luhithi wakilia,njiani kwenda Horonaimu wanatoa kilio cha maangamizi.

6. Kijito cha Nimrimu kimekauka;nyasi zimekauka, majani mabichi yamenyauka,hakuna chochote kinachoota hapo.

7. Watu wanavuka kijito cha Mierebiwamebeba mali yao yote waliyochuma,na kila walichojiwekea kama akiba.

8. Kilio kimezuka pote nchini Moabu,maombolezo yao yamefika Eglaimu,naam, yamefika mpaka Beer-elimu.

9. Maji ya Diboni yamejaa damu,lakini Mungu ataongeza msiba wa Diboni.Hao wachache watakaobaki haina kukimbia kutoka nchini Moabu,watapelekewa simba wa kuwaua.