Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52
  53. 53
  54. 54
  55. 55
  56. 56
  57. 57
  58. 58
  59. 59
  60. 60
  61. 61
  62. 62
  63. 63
  64. 64
  65. 65
  66. 66

Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 19 Biblia Habari Njema (BHN)

Mungu ataiadhibu nchi ya Misri

1. Kauli ya Mungu dhidi ya nchi ya Misri.“Mwenyezi-Mungu amepanda juu ya wingu liendalo kasina kuja mpaka nchi ya Misri.Sanamu za miungu ya Wamisri zitatetemeka mbele yake,mioyo ya Wamisri itayeyuka kwa hofu.

2. Mimi nitawachochea Wamisri wagongane:Ndugu na ndugu yake,jirani na jirani yake,mji mmoja na mji mwingine,mfalme mmoja na mfalme mwingine.

3. Nitawaondolea Wamisri uhodari wao,nitaivuruga mipango yao;watatafuta maoni kwa sanamu na mizimu,wachawi, mizuka na pepo.

4. Nitawatia Wamisri mikononi mwa bwana katili,mfalme mkali ambaye atawatawala.Mimi Bwana Mwenyezi-Mungu wa majeshi, nimenena.”

5. Maji ya mto Nili yatakaushwa,nao utakauka kabisa.

6. Mifereji yake itatoa uvundo,vijito vyake vitapunguka na kukauka.Nyasi na mafunjo yake yataoza.

7. Sehemu za kandokando ya Nili zitakuwa tupu.Mimea yote iliyopandwa humo itakaukana kupeperushiwa mbali na kutoweka.

8. Wavuvi watalia na kuomboleza,wote watumiao ndoana watalalama;wote wanaotanda nyavu majini watakufa moyo.

9. Wafuma nguo za kitani watakata tamaa,wote kwa pamoja watakufa moyo.

10. Wafuma nguo watafedheheshwa,na vibarua watahuzunika.

11. Viongozi wa mji wa Soani ni wapumbavu kabisa,washauri wa Farao wanatoa shauri la kijinga!Awezaje kila mmoja kumwambia Farao,“Mimi ni mzawa wa mtaalamu stadi;mzawa wa wafalme wa hapo kale!”

12. Wako wapi, ewe Farao, wataalamu wako?Waache basi wakuambie na kukujulishaaliyopanga Mwenyezi-Mungu wa majeshi dhidi ya Misri!

13. Lakini viongozi wa Soani ni wapumbavu,wakuu wa Memfisi wamedanganyika.Hao walio msingi wa makabila yaowamelipotosha taifa la Misri.

14. Mwenyezi-Mungu amewamwagia hali ya vurugu,wakawapotosha Wamisri katika mipango yao yote,wakawa kama mlevi anayeyumbayumba akitapika.

15. Hakuna mtu yeyote nchini Misri,kiongozi au raia, mashuhuri au duni,awezaye kufanya lolote la maana.

Wamisri watamwabudu Mwenyezi-Mungu

16. Siku ile watu wa Misri wataogopa kama wanawake. Watatetemeka kwa hofu watakapomwona Mwenyezi-Mungu wa majeshi ameunyosha mkono wake dhidi yao.

17. Yuda atakuwa tishio kubwa kwa Wamisri. Wote watakaoambiwa habari za Yuda wataingiwa na woga kwa sababu ya jambo aliloamua Mwenyezi-Mungu wa majeshi kuwatenda.

18. Siku hiyo lugha ya Kiebrania itatumika katika miji mitano ya Misri, na watu wa miji hiyo wataapa kuwa waaminifu kwa Mwenyezi-Mungu wa majeshi. Mji mmojawapo utaitwa “Mji wa Jua.”

19. Siku hiyo, kutakuwa na madhabahu kwa ajili ya Mwenyezi-Mungu katikati ya nchi ya Misri, na nguzo iliyowekwa wakfu kwa Mungu kwenye mpaka wa Misri.

20. Madhabahu hiyo itakuwa ishara na ushuhuda kwake Mwenyezi-Mungu wa majeshi katika nchi ya Misri. Watu wakimlilia Mwenyezi-Mungu humo kwa sababu ya kukandamizwa, yeye atawapelekea mkombozi atakayewatetea na kuwakomboa.

21. Mwenyezi-Mungu atajijulisha kwa Wamisri na hapo ndipo Wamisri watakapomkiri na kumwabudu kwa kumtolea tambiko na sadaka za kuteketezwa. Hali kadhalika, watamwekea Mwenyezi-Mungu nadhiri ambazo watazitimiza.

22. Mwenyezi-Mungu atawaadhibu Wamisri na kuwaponya. Nao watamrudia, naye atayasikiliza maombi yao na kuwaponya.

23. Wakati huo, kutakuwa na barabara kuu kutoka nchi ya Misri hadi nchi ya Ashuru. Waashuru watawatembelea Wamisri, na Wamisri watawatembelea Waashuru; nao wote watamwabudu Mungu pamoja.

24. Wakati huo, Israeli itahesabiwa pamoja na Misri na Ashuru; mataifa haya matatu yatakuwa baraka kwa dunia yote.

25. Mwenyezi-Mungu wa majeshi atawabariki na kusema, “Wabarikiwe Wamisri watu wangu, kadhalika na Waashuru ambao ni ishara ya kazi yangu na Waisraeli walio mali yangu.”