Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52
  53. 53
  54. 54
  55. 55
  56. 56
  57. 57
  58. 58
  59. 59
  60. 60
  61. 61
  62. 62
  63. 63
  64. 64
  65. 65
  66. 66

Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 65 Biblia Habari Njema (BHN)

Mungu huwaadhibu waasi

1. Mwenyezi-Mungu asema;“Nilikuwa tayari kujioneshakwao wasiouliza habari zangu.Nilikuwa tayari kuwapokeawale wasionitafuta.Nililiambia taifa ambalo halikuomba kwa jina langu:‘Nipo hapa! Nipo hapa!’

2. Mchana kutwa niliwanyoshea mikono watu waasi,watu ambao hufuata njia zisizo sawa,watu ambao hufuata fikira zao wenyewe.

3. Ni watu ambao daima hunichokoza waziwazi;hutambikia miungu yao katika bustani,na kuifukizia ubani juu ya matofali.

4. Huketi makaburini na kukaa mafichoni usiku.Hula nyama ya nguruwe na mchuzi wa wanyama haramu.

5. Huwaambia wale wanaokutana nao:‘Kaeni mbali nami;msinikaribie kwani mimi ni mtakatifu!’Watu hao wananikasirisha mno,hasira yangu ni kama moto usiozimika.

6. “Jueni kuwa nimelitia jambo hilo moyoni,sitanyamaza bali nitawafanya walipe;nitawafanya walipe kwa wingi.

7. Mimi Mwenyezi-Mungu, nitawalipiza maovu yaowayalipie na maovu ya wazee wao.Wao waliifukizia ubani miungu yao milimani,wakanitukana mimi huko vilimani.Nitawafanya walipe kwa wingi,watayalipia matendo yao ya awali.”

8. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Mtu akikuta kishada cha zabibu nzuri,watu husema: ‘Tusikiharibu; kina baraka.’Ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu;sitawaangamiza wote.

9. Nitawajalia watu wa Yakobo,na Yuda nitamjalia warithi wa milima yangu;watumishi wangu watakaa huko.

10. Nchi tambarare ya Sharoni itakuwa malisho,bonde la Akori litakuwa mapumziko ya mifugokwa ajili ya watu wangu walionitafuta.

11. “Lakini nitafanya nini na nyinyimnaoniacha mimi Mwenyezi-Mungu,msioujali Siyoni, mlima wangu mtakatifu,nyinyi mnaoabudu mungu ‘Gadi’,na kumtolea tambiko ya divai mungu ‘Meni’?

12. Nimewapangia kifo kwa upanga,nyote mtaangukia machinjoni!Maana, nilipowaita, hamkuniitikia;niliponena, hamkunisikiliza.Mlitenda yaliyo maovu mbele yangu,mkachagua yale nisiyoyapenda.

13. Basi, mimi Mwenyezi-Mungu nasema,watumishi wangu watakula,lakini nyinyi mtaona njaa;watumishi wangu watakunywa,lakini nyinyi mtaona kiu;watumishi wangu watafurahi,lakini nyinyi mtafedheheka.

14. Watumishi wangu wataimba kwa furaha moyoni,lakini nyinyi mtalia kwa uchungu moyonina kupiga kelele kwa uchungu mkubwa rohoni.

15. Wale niliowachagua nitawapa jina jipya.Lakini nyinyi jina lenu watalitumia kulaania;‘Watasema: Bwana Mungu awaue kama hao.’

16. Basi, mwenye kujitakia baraka nchini,atajitakia baraka kwa Mungu wa kweli.Mwenye kuapa katika nchi hii,ataapa kwa Mungu wa kweli.Maana taabu za zamani zimepitazimetoweka kabisa mbele yangu.

Ulimwengu mpya

17. “Sasa, naumba mbingu mpya na dunia mpya.mambo ya zamani hayatakumbukwa tena.

18. Furahini, mkashangilie milele,kwa ajili ya vitu hivi ninavyoumba.Yerusalemu nitaufanya mji wa shangwe,na watu wake watu wenye furaha.

19. Nami nitaufurahia mji wa Yerusalemu,nitawafurahia watu wangu.Sauti ya kilio haitasikika tena,kilio cha taabu hakitakuwako.

20. Hakutakuwa tena na vifo vya watoto wachanga,wazee nao hawatakufa kabla ya wakati wao.Akifa mtu wa miaka 100 amekufa akiwa kijana;na akifa kabla ya miaka 100 ni balaa.

21. Watu watajenga nyumba na kuishi humo;watalima mizabibu na kula matunda yake.

22. Hawatajenga nyumba zikaliwe na watu wengine,wala kulima chakula kiliwe na watu wengine.Maana watu wangu niliowachaguawataishi maisha marefu kama miti;wateule wangu watafurahia matunda ya jasho lao.

23. Kazi zao hazitakuwa bure,wala hawatazaa watoto wa kupata maafa;maana watakuwa waliobarikiwa na Mwenyezi-Mungu,wamebarikiwa wao pamoja na wazawa wao.

24. Hata kabla hawajaniita, mimi nitawaitikia;kabla hawajamaliza kusema, nitakuwa nimewajibu.

25. Mbwamwitu na kondoo watakula pamoja,simba watakula nyasi kama ng'ombe,nao nyoka chakula chao kitakuwa vumbi.Katika mlima wangu wote mtakatifu,hakuna atakayeumiza au kuharibu kitu.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”