Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52
  53. 53
  54. 54
  55. 55
  56. 56
  57. 57
  58. 58
  59. 59
  60. 60
  61. 61
  62. 62
  63. 63
  64. 64
  65. 65
  66. 66

Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 27 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Siku hiyo, Mwenyezi-Mungu atautwaa upanga wake mkubwa, mkali na imara, na kuliadhibu dude Lewiyathani joka lirukalo na danganyifu; Mwenyezi-Mungu ataliua joka liishilo baharini.

2. Siku hiyo, Mwenyezi-Mungu atasema hivi:“Imbeni utenzi wa shamba langu zuri la mizabibu!

3. Mimi, Mwenyezi-Mungu, ni mkulima wake;nalimwagilia maji kila wakati,ninalilinda usiku na mchana,lisije likaharibiwa na mtu yeyote.

4. Silikasirikii tena shamba hili;kama miiba na mbigili ingelilivamia,mimi ningepambana nayo na kuichoma moto.

5. Maadui za watu wangu wakitaka ulinzi wangu,basi, na wafanye amani nami;naam, wafanye amani nami.”

6. Itakuja siku wazawa wa Yakobo watashika mizizi;naam, watu wa Israeli watachanua na kuchipua,na kuijaza dunia yote kwa matunda.

7. Mungu hakuwaadhibu Waisraeli vikalikama alivyowaadhibu maadui wake;Waisraeli waliopotea vitani,ni wachache kuliko wale wa maadui zake.

8. Aliwaadhibu watu wake kwa kuwapeleka uhamishoni.Wakati wa upepo mkali wa mashariki,aliwaondoa kwa kipigo kikali.

9. Hivi ndivyo uovu wa wazawa wa Yakobo utakavyoondolewa,hivi ndivyo dhambi yake itakavyofutwa kabisa:Ataziharibu madhabahu za miungu;mawe yake yatasagwasagwa kama chokaa;Ashera, wala madhabahu za kufukizia ubani hazitabaki.

10. Mji ule wa ngome sasa umekuwa mtupu,umeachwa na kuhamwa kama jangwa,humo ndama wanalisha na kupumzika.

11. Matawi ya miti yamekauka na kuvunjika;kina mama huyaokota wakawashia moto.Watu hawa hawajaelewa kitu,kwa hiyo Mungu, Muumba wao, hatawahurumia,yeye aliyewafanya, hatawafadhili.

12. Siku hiyo, kutoka mto Eufrate hadi mpakani mwa Misri, Mwenyezi-Mungu ataipura nafaka yake, nanyi Waisraeli mtakusanywa mmojammoja.

13. Siku hiyo, tarumbeta kubwa itapigwa na watu wote wa Israeli waliopotea nchini Ashuru au waliotawanywa nchini Misri watarudi na kumwabudu Mwenyezi-Mungu juu ya mlima mtakatifu huko Yerusalemu.