Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52
  53. 53
  54. 54
  55. 55
  56. 56
  57. 57
  58. 58
  59. 59
  60. 60
  61. 61
  62. 62
  63. 63
  64. 64
  65. 65
  66. 66

Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 9 Biblia Habari Njema (BHN)

Mtoto amezaliwa kwetu

1. Lakini nchi ile iliyokuwa imekumbwa na huzuni haitabaki daima katika giza hilo kuu. Hapo awali Mungu alizifedhehesha nchi za Zebuluni na Naftali, lakini siku za usoni ataifanikisha sehemu hii ya baharini na nchi iliyo ngambo ya Yordani na hata Galilaya wanamoishi watu wa mataifa.

2. Watu waliotembea gizaniwameona mwanga mkubwa.Watu walioishi katika nchi ya giza kuu,sasa mwanga umewaangazia.

3. Wewe, ee Mungu, umelikuza taifa,umeiongeza furaha yake.Watu wanafurahi mbele yako,wana furaha kama wakati wa mavuno,kama wafurahivyo wanaogawana nyara.

4. Maana nira nzito walizobeba,nira walizokuwa wamefungwa,na fimbo ya wanyapara wao,umezivunjavunja kama wakati wa Wamidiani.

5. Viatu vyote vya washambulizi vitanina mavazi yote yenye madoa ya damuyatateketezwa kama kuni za kuwasha moto.

6. Maana mtoto amezaliwa kwa ajili yetu,tumepewa mtoto wa kiume.Naye atapewa mamlaka ya kutawala.Ataitwa: “Mshauri wa Ajabu”.“Mungu Mwenye Nguvu”,“Baba wa Milele”,“Mfalme wa Amani”.

7. Utawala wake utastawi daima,amani ya ufalme wake haitakoma.Atachukua wadhifa wa mfalme Daudina kutawala juu ya ufalme wake;ataustawisha na kuuimarisha,kwa haki na uadilifu,tangu sasa na hata milele.Hayo atayafanya Mwenyezi-Mungu wa majeshi.

Adhabu ya Waisraeli

8. Mwenyezi-Mungu ametoa tamko dhidi ya Yakobonalo litampata Israeli.

9. Watu wote watatambua,ukoo wote wa Efraimuna wakazi wa Samaria.Kwa kiburi na majivuno wanasema:

10. “Kuta za matofali zimeangukalakini sisi tutazijenga kwa mawe yaliyochongwa!Nyumba za boriti za mikuyu zimeharibiwalakini mahali pake tutajenga za mierezi.”

11. Basi, Mwenyezi-Mungu atawaletea wapinzanina kuwachochea maadui zao.

12. Waaramu upande wa mashariki,Wafilisti upande wa magharibi,wamepanua vinywa vyao kuimeza Israeli.Hata hivyo, hasira yake haijatulia,bado ameunyosha mkono wake.

13. Ingawa aliwaadhibu watu,hawakumrudia Mwenyezi-Mungu wa majeshi.

14. Basi kwa muda wa siku moja tu,Mwenyezi-Mungu atakata katika Israeli vichwa na mikia,tawi la mtende na nyasi:

15. Vichwa ndio wazee na waheshimiwa,mikia ndio manabii wafundishao uongo.

16. Wale wanaoongoza watu hawa wamewapotosha,na hao wanaoongozwa nao wamepotoka.

17. Kwa hiyo, Mwenyezi-Mungu hawahurumii vijana wao,hana huruma juu ya yatima na wajane wao;kwani hakuna hata mmoja amchaye Mungu,kila mtu husema uongo.Hata hivyo, hasira yake haijatulia,bado ameunyosha mkono wake.

18. Uovu huwaka kama motouteketezao mbigili na miiba;huwaka kama moto msituni,na kutoa moshi mzito upandao angani juu.

19. Kwa ghadhabu ya Mwenyezi-Mungu wa majeshinchi imechomwa moto,na watu ni kama kuni za kuuwasha.Hakuna mtu anayemhurumia ndugu yake;

20. wananyanganya upande mmoja na hawatosheki;wanakula upande mwingine lakini hawashibi.Kila mmoja anamshambulia mwenzake.

21. Manase dhidi ya Efraimu,Efraimu dhidi ya Manasena wote wawili dhidi ya Yuda.Hata hivyo, hasira ya Mwenyezi-Mungu haijatulia,bado ameunyosha mkono wake.