Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52
  53. 53
  54. 54
  55. 55
  56. 56
  57. 57
  58. 58
  59. 59
  60. 60
  61. 61
  62. 62
  63. 63
  64. 64
  65. 65
  66. 66

Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 33 Biblia Habari Njema (BHN)

Maafa kwa mwangamizi

1. Ole wako ewe mwangamizi,unayeangamiza bila wewe kuangamizwa!Ole wako wewe mtenda hila,ambaye hakuna aliyekutendea hila!Utakapokwisha kuangamizawewe utaangamizwa!Utakapomaliza kuwatendea watu hilawewe utatendewa hila.

2. Ee Mwenyezi-Mungu, utuonee huruma,kwako tumeliweka tumaini letu.Uwe kinga yetu kila siku,wokovu wetu wakati wa taabu.

3. Kwa kishindo cha sauti yako watu hukimbia;unapoinuka tu, mataifa hutawanyika.

4. Maadui zao wanakusanya mateka,wanayarukia kama panzi.

5. Mwenyezi-Mungu ametukuka,yeye anaishi juu mbinguni.Ameujaza Siyoni haki na uadilifu.

6. Enyi watu wa Yerusalemu,Mwenyezi-Mungu atawajalieni usalama,atawaokoa na kuwapa hekima na maarifa.Hazina yenu kuu ni kumcha Mwenyezi-Mungu.

7. Haya, mashujaa wao wanalia,wajumbe wa amani wanaomboleza.

8. Barabara kuu zimebaki tupu;hamna anayesafiri kupitia humo.Mikataba inavunjwa ovyo,mashahidi wanadharauliwa.Hamna anayejali tena maisha ya binadamu.

9. Nchi inaomboleza na kunyauka;misitu ya Lebanoni imekauka,bonde zuri la Sharoni limekuwa jangwa,huko Bashani na mlimani Karmelimiti imepukutika majani yake.

Mwenyezi-Mungu awaonya maadui zake

10. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Sasa mimi nitainuka;sasa nitajiweka tayari;sasa mimi nitatukuzwa.

11. Mipango yenu yote ni kama makapi,na matokeo yake ni takataka tupu.Pumzi yangu itawaangamiza kama moto.

12. Watu watakuwa kama wamechomwa kuwa majivu,kama miiba iliyokatwa na kuteketezwa motoni.

13. Sikilizeni mambo mliyofanya enyi mlio mbali,nanyi mlio karibu kirini uwezo wangu.”

14. Wenye dhambi katika Siyoni wanaogopa,wasiomcha Mungu wanatetemeka na kusema:“Nani awezaye kuukaribia moto huu mkali?Nani awezaye kustahimili miali ya moto wa milele?”

15. Ni mtu aishiye kwa uadilifu na asemaye ukweli;mtu anayedharau kabisa utajiri wa dhuluma,anayekataa hongo kata kata,asiyekubali kamwe kusikia mipango ya mauaji,wala hakubali macho yake yaone maovu.

16. Mtu wa namna hiyo anaishi juu,mahali salama penye ngome na miamba;chakula chake atapewa daima,na maji yake ya kunywa hayatakosekana.

Wakati mzuri ujao

17. Mtaweza kumwona mfalme katika fahari yake,mtaiona nchi anayotawala, kubwa na pana.

18. Mtafikiria tisho lililopita na kujiuliza,“Wako wapi wale waliokadiria na kukisia kodi?Wako wapi wale waliopeleleza ulinzi wetu?”

19. Hamtawaona tena watu wale wenye kiburi,wanaozungumza lugha isiyoeleweka.

20. Tazameni Siyoni tunamofanya sikukuu zetu;tazameni mji Yerusalemu, makao matulivu, hema imara;vigingi vyake havitangolewa kamwe,kamba zake hazitakatwa hata moja.

21. Humo Mwenyezi-Mungu atatuonesha ukuu wake.Kutakuwa na mito mikubwa na vijito,ambamo meli za vita hazitapita,wala meli kubwa kuingia.

22. Maana Mwenyezi-Mungu ni hakimu wetu,yeye ni mtawala wetu;Mwenyezi-Mungu ni mfalme wetu,yeye ndiye anayetuokoa.

23. Ewe Siyoni, kamba zako zimelegea,haziwezi kushikilia matanga yake,wala kuyatandaza.Lakini nyara nyingi zitagawanywa;hata vilema wataweza kuchukua sehemu yao.

24. Hakuna atakayesema tena ni mgonjwa;watu watasamehewa uovu wao wote.