Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31

Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 5 Biblia Habari Njema (BHN)

Onyo dhidi ya uasherati

1. Mwanangu, sikia hekima yangu,tega sikio usikilize elimu yangu.

2. Ndipo utakapoweza kuhifadhi busara,na midomo yako izingatie maarifa.

3. Mdomo wa mwanamke mpotovu ni mtamu kama asali,maneno yake ni laini kuliko mafuta;

4. lakini hatimaye ni mchungu kama pakanga,ni mkali kama upanga wenye makali kuwili.

5. Nyayo zake zaelekea chini mautini,hatua zake zaenda kuzimu.

6. Yeye haijali njia ya uhai,njia zake ni za kutangatanga, wala hajui.

7. Sasa enyi wanangu, nisikilizeni,wala msisahau maneno ya kinywa changu.

8. Iepushe njia yako mbali naye,wala usiukaribie mlango wa nyumba yake.

9. Usije ukawapa wengine heshima yako,na wakatili miaka yako;

10. wageni wasije wakajishibisha kwa mali yako,na jasho lako likaishia nyumbani kwa mgeni.

11. Mwishoni mwa maisha yako utaombolezawakati mwili wako utakapoangamizwa.

12. Hapo utasema, “Jinsi gani nilivyochukia nidhamu,na kudharau maonyo moyoni mwangu!

13. Sikuisikiliza sauti ya waalimu wangu,wala kuwategea sikio wakufunzi wangu.

14. Sasa niko karibu kuangamia kabisambali na jumuiya ya watu.”

15. Mkeo ni kama kisima cha maji safi:Kunywa maji ya kisima chako mwenyewe.

16. Ya nini chemchemi zako zitawanywe mbali,na vijito vya maji barabarani?

17. Hiyo ni yako wewe mwenyewe,wala usiwashirikishe watu wengine.

18. Chemchemi yako na ibarikiwe,umfurahie mke uliyemwoa ukiwa kijana.

19. Ni mzuri kama ayala, apendeza kama paa.Mahaba yake yakufurahishe kila wakati,umezwe daima na pendo lake.

20. Mwanangu, ya nini kutekwa na mwanamke mwasherati?Ya nini kumkumbatia kifuani mwanamke mgeni?

21. Kumbuka njia za mtu zi wazi mbele ya Mwenyezi-Mungu;yeye anaona kila hatua anayochukua binadamu.

22. Mtu mwovu hunaswa kwa uovu wake mwenyewe;hukamatwa katika tanzi za dhambi yake mwenyewe.

23. Yeye hufa kwa utovu wa nidhamu,huangamia kwa sababu ya upuuzi wake mkuu.