Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31

Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 25 Biblia Habari Njema (BHN)

Methali zaidi za Solomoni

1. Hizi nazo ni methali nyingine za mfalme Solomoni walizonakili watu wa Hezekia, mfalme wa Yuda.

2. Mungu hutukuzwa kwa kuficha mambo,lakini mfalme hutukuzwa kwa yale anayoeleza.

3. Kama zilivyo mbali mbingu na kirefu kina cha ardhindivyo zisivyochunguzika akili za mfalme.

4. Toa takataka katika fedha,na mhunzi atakutengenezea chombo kizuri.

5. Waondoe waovu mbele ya mfalme,na utawala wake utaimarika katika haki.

6. Usijipendekeze kwa mfalme,wala usijifanye mtu mkubwa,

7. maana ni heri kuambiwa, “Njoo huku mbele”,kuliko kuporomoshwa mbele ya mkuu.Mambo uliyoyaona kwa macho yako,

8. usiharakishe kuyapeleka mahakamani;maana utafanya nini hapo baadaye,shahidi mwingine akibatilisha hayo usemayo?

9. Suluhisha ugomvi na mwenzako peke yake,na kila mmoja wenu asitoe siri ya mwenzake;

10. watu wasije wakajua kuna siri,ukajiharibia jina lako daima.

11. Neno lisemwalo wakati unaofaa,ni kama nakshi za dhahabu juu ya madini ya fedha.

12. Onyo la mwenye hekima kwa mtu msikivu,ni bora kuliko pete au vito vya dhahabu safi.

13. Mjumbe mwaminifu humfurahisha yule aliyemtuma,kama maji baridi wakati wa joto la mavuno.

14. Kama vile mawingu na upepo bila mvua,ndivyo alivyo mtu anayejigamba kutoa zawadi asiitoe.

15. Kwa uvumilivu mtawala huweza kushawishika;ulimi laini huvunja mifupa.

16. Upatapo asali kula kiasi cha kukutosha,usije ukaikinai na kuitapika.

17. Usimtembelee jirani yako mara kwa mara,usije ukamchosha naye akakuchukia.

18. Mtu atoaye ushahidi wa uongo dhidi ya mwenziwe,ni hatari kama rungu, upanga au mshale mkali.

19. Kumtegemea mtu asiyeaminika wakati wa taabu,ni kama jino bovu au mguu ulioteguka.

20. Kumwimbia mtu mwenye huzuni,ni kama kuvua nguo wakati wa baridi,au kutia siki katika kidonda.

21. Adui yako akiwa na njaa, mpe chakula;akiwa na kiu, mpe maji ya kunywa.

22. Hivyo utafanya apate aibu kali,kama makaa ya moto kichwani pake,naye Mwenyezi-Mungu atakutuza.

23. Upepo wa kusi huleta mvua,hali kadhalika masengenyo huleta chuki.

24. Afadhali kuishi pembeni juu ya paa,kuliko kuishi nyumbani pamoja na mwanamke mgomvi.

25. Kama vile maji baridi kwa mwenye kiu,ndivyo habari njema kutoka mbali.

26. Mwadilifu akubaliye kufuata mambo ya mwovu,ni chemchemi iliyochafuliwa au kisima kilichotibuliwa.

27. Si vizuri kula asali nyingi mno;kadhalika haifai kujipendekeza mno.

28. Mtu asiyeweza kuzuia hasira yake,ni kama mji usio na ulinzi unaposhambuliwa.