Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31

Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 11 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mizani ya udanganyifu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,lakini matumizi ya kipimo halali ni furaha kwake.

2. Kiburi huandamana na fedheha,lakini kwa watu wanyenyekevu mna hekima.

3. Unyofu wa watu wema huwaongoza,upotovu wa wenye hila huwaangamiza.

4. Utajiri haufai kitu siku ya ghadhabu,lakini uadilifu huokoa kutoka kifo.

5. Uadilifu wa watu wanyofu huinyosha njia yao,lakini waovu huanguka kwa uovu wao wenyewe.

6. Uadilifu wa wanyofu huwaokoa na hatari,lakini wafitini hunaswa kwa tamaa zao wenyewe.

7. Mwovu akifa tumaini lake nalo hutoweka;tazamio la asiyemcha Mungu huishia patupu.

8. Mtu mnyofu huokolewa katika shida,na mwovu huingia humo badala yake.

9. Asiyemcha Mungu huangamiza wengine kwa mdomo wake,lakini mwadilifu huokolewa kwa maarifa yake.

10. Waadilifu wakipata fanaka mji hushangilia,na waovu wakiangamia watu hupiga vigelegele.

11. Mji hufanikishwa kwa baraka za wanyofu,lakini huangamizwa kwa mdomo wa waovu.

12. Anayemdharau jirani yake hana akili,mtu mwenye busara hukaa kimya.

13. Apitapitaye akichongea hutoa siri,lakini anayeaminika rohoni huficha siri.

14. Pasipo na uongozi taifa huanguka,penye washauri wengi pana usalama.

15. Anayemdhamini mgeni atakuja juta,lakini anayechukia mambo ya dhamana yu salama.

16. Mwanamke mwema huheshimiwa,mwanamume mwenye bidii hutajirika.

17. Mtu mkarimu hufaidika yeye mwenyewe,lakini mtu mkatili hujiumiza mwenyewe.

18. Faida anayopata mwovu ni ya uongo,lakini atendaye mema hakika atapata faida ya kweli.

19. Mtu anayepania kuwa mwadilifu ataishi,lakini anayechagua kutenda maovu atakufa.

20. Wenye nia mbaya ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,lakini wenye mwenendo mwema ni furaha yake.

21. Hakika mwovu hataepa kuadhibiwa,lakini waadilifu wataokolewa.

22. Mwanamke mzuri asiye na akili,ni kama pete ya dhahabu puani mwa nguruwe.

23. Matazamio ya waadilifu yana matokeo mema;tamaa za waovu huishia katika ghadhabu.

24. Atoaye kwa ukarimu huzidi kutajirika;lakini bahili huzidi kudidimia katika umaskini.

25. Mtu mkarimu atafanikishwa,amnyweshaye mwingine maji naye atanyweshwa.

26. Watu humlaani afichaye nafaka,lakini humtakia baraka mwenye kuiuza.

27. Atafutaye kutenda mema hupata fadhili,lakini atafutaye kutenda maovu atapatwa na maovu.

28. Anayetegemea mali zake ataanguka,lakini mwadilifu atastawi kama jani bichi.

29. Anayeivunja nyumba yake ataambua upepo.Mpumbavu atakuwa mtumwa wa wenye hekima.

30. Matendo ya mwadilifu huleta uhai,lakini uhalifu huuondoa uhai.

31. Ikiwa mwadilifu hupata tuzo hapa duniani,hakika mwovu na mwenye dhambi atapatilizwa.