Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31

Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 27 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Usijisifie ya kesho,hujui nini kitatokea leo mpaka kesho.

2. Acha watu wengine wakusifu,kuliko mdomo wako wewe mwenyewe.

3. Jiwe ni zito na mchanga kadhalika,lakini usumbufu wa mpumbavu ni mzito zaidi.

4. Ghadhabu ni katili na hasira huangamiza;lakini ni nani awezaye kuukabili wivu?

5. Afadhali mtu anayekuonya waziwazi,kuliko yule afichaye upendo.

6. Makaripio ya rafiki yaonesha uaminifu,lakini busu la adui ni udanganyifu.

7. Aliyeshiba hata asali huikataa,lakini kwa mwenye njaa kila kichungu ni kitamu.

8. Mtu aliyepotea mbali na kwake,ni kama ndege aliyepotea mbali na kiota chake.

9. Mafuta na manukato huufurahisha moyo,lakini taabu hurarua roho.

10. Usisahau rafiki zako wala wa baba yako.Ukipatwa na janga usikimbilie kwa nduguyo;afadhali jirani aliye karibu kuliko ndugu aliye mbali.

11. Uwe na hekima mwanangu upate kunifurahisha moyo,nami sitakosa la kumjibu yeyote anayenilaumu.

12. Mwenye busara huona hatari akajificha,lakini mjinga hujitokeza mbele akaumia.

13. Mtu akiahidi mbele yako kumdhamini mgeni, chukua nguo yake;mfanye awajibike kwa kuwadhamini wageni.

14. Amwamkiaye jirani kwa kelele alfajiri,itaeleweka kwamba amemtakia laana.

15. Mke mgomvi daima,ni sawa na tonatona ya maji siku ya mvua.

16. Kumzuia ni sawa na kuzuia upepo,au kukamata mafuta kwa mkono.

17. Chuma hunoa chuma,kadhalika mtu hufundishwa na wenzake.

18. Anayeutunza mtini hula tini,anayemhudumia bwana wake ataheshimiwa.

19. Kama uso ujionavyo wenyewe majini,ndivyo ujijuavyo mwenyewe moyoni.

20. Kuzimu na Uharibifu kamwe havishibi,kadhalika na macho ya watu hayashibi.

21. Ubora wa fedha au dhahabu hupimwa kwa moto,na mtu hupimwa kutokana na sifa zake.

22. Mtwange mpumbavu katika kinu pamoja na nafaka,lakini hutafaulu kumtenganisha na upumbavu wake.

23. Angalia vizuri hali ya mifugo yako;tunza vizuri wanyama wako.

24. Maana utajiri haudumu milele,wala taji haidumu vizazi vyote.

25. Baada ya kukata nyasi na kuzihifadhi,kata majani toka milimani,huku nyasi zinachipua upya.

26. Kondoo watakupatia sufu kwa mavazi,mbuzi nao utauza na kujinunulia mashamba;

27. watakupa maziwa ya kukutosha wewe na jamaa yako,na kwa ajili ya watumishi wako wa kike.