Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31

Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 4 Biblia Habari Njema (BHN)

Manufaa ya hekima

1. Wanangu, sikilizeni mwongozo wa baba yenu,tegeni sikio mpate kuwa na akili.

2. Maana ninawapa maagizo mema,msiyakatae mafundisho yangu.

3. Mimi pia nilikuwa mtoto mwenye baba,nilikuwa mpole, kipenzi cha mama yangu.

4. Baba yangu alinifundisha hiki:“Zingatia kwa moyo maneno yangu,shika amri zangu nawe utaishi.

5. Jipatie hekima, jipatie ufahamu;usisahau wala kupuuza maneno yangu.

6. Usimwache Hekima, naye atakutunza;umpende, naye atakulinda.

7. Jambo la msingi ni kujipatia hekima;toa vyote ulivyonavyo ujipatie akili.

8. Mthamini sana Hekima, naye atakutukuza;ukimshikilia atakupa heshima.

9. Atakuvika kilemba kizuri kichwani pako,atakupa taji maridadi.”

10. Mwanangu, sikia na kuyapokea maneno yangu,ili upate kuwa na miaka mingi ya kuishi.

11. Nimekufundisha njia ya hekima,nimekuongoza katika njia nyofu.

12. Ukitembea hatua zako hazitazuiwa,wala ukikimbia hutajikwaa.

13. Zingatia mafundisho ya Hekima na usimwache aponyoke,mshike kwa makini maana yeye ni uhai wako.

14. Usijiingize katika njia ya waovu,wala usifuate mwenendo wa watu wabaya.

15. Iepe njia hiyo wala usiikaribie;jiepushe nayo, uende zako.

16. Waovu kamwe hawalali wasipotenda uovu;hawapati usingizi wasipomkwaza mtu.

17. Maana uovu ndicho chakula chao,ukatili ndiyo divai yao.

18. Njia ya watu wema ni kama nuru ya alfajiri,ambayo hungaa zaidi na zaidi hata mchana kamili.

19. Lakini njia ya waovu ni kama giza nene,hawajui kinachowafanya wajikwae.

20. Mwanangu, sikiliza kwa makini maneno yangu,itegee sikio misemo yangu.

21. Usiyaache yatoweke machoni pako,yahifadhi ndani ya moyo wako.

22. Maana hayo ni uhai kwa mtu anayeyapata,ni dawa kwa mwili wake wote.

23. Linda moyo wako kwa uangalifu wote,maana humo zatoka chemchemi za uhai.

24. Tenga mbali nawe lugha potovu;wala midomo yako isitamke maneno madanganyifu.

25. Uyaelekeze macho yako mbele kwa ujasiri,mtazamo wako uwe mbele moja kwa moja.

26. Fikiria njia utakayochukua,na hatua zako zote zitakuwa kamili.

27. Usigeukie kulia wala kushoto;epusha mguu wako mbali na uovu.