Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31

Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 23 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Ukiketi kula pamoja na mtawala,usisahau hata kidogo uko pamoja na nani.

2. Zuia sana hamu yako,ikiwa wewe wapenda sana kula.

3. Usitamani vyakula vyake vizuri,maana vyaweza kukudanganya.

- 7 -

4. Ikiwa unayo hekima ya kutosha,usijitaabishe kutafuta utajiri.

5. Kufumba na kufumbua utajiri hutoweka,huwa kama umepata mabawa ghafla,ukaruka na kutowekea angani kama tai.

- 8 -

6. Usile chakula cha mtu bahili,wala usitamani mapochopocho yake,

7. maana moyoni mwake anahesabu unachokula.Atakuambia, “Kula, kunywa!”Lakini moyoni mwake hayuko pamoja nawe.

8. Utatapika vipande ulivyokula;shukrani zako zote zitakuwa za bure.

- 9 -

9. Usiseme maneno yako mbele ya mpumbavu,maana atapuuza hekima ya maneno yako.

- 10 -

10. Usiondoe alama ya mpaka wa zamani,wala usiingilie mashamba ya yatima,

11. maana Mungu, Mkombozi, ni mwenye nguvu,naye ataitetea haki yao dhidi yako.

- 11 -

12. Tumia akili zako kufuata mafundisho;tumia masikio yako kusikiliza maarifa.

- 12 -

13. Usiache kumrudi mtoto;ukimchapa kiboko hatakufa.

14. Ukimtandika kiboko,utayaokoa maisha yake na kuzimu.

- 13 -

15. Mwanangu, moyo wako ukiwa wenye busara,moyo wangu pia utakuwa wenye furaha.

16. Moyo wangu utashangilia,mdomo wako utakaposema maneno yaliyo sawa.

- 14 -

17. Moyo wako usiwaonee wivu wenye dhambi,ila endelea kumcha Mwenyezi-Mungu siku zote.

18. Hakika kuna kesho ya milele,na tumaini lako halitakuwa bure.

- 15 -

19. Sikia mwanangu, uwe na hekima;fikiria sana jinsi unavyoishi.

20. Usiwe mmoja wa walevi wa divai,wala walafi wenye kupenda nyama,

21. maana walevi na walafi wataishia kuwa maskini,anayetumia siku yake kusinzia atavaa matambara.

- 16 -

22. Msikilize baba yako aliyekuzaa,wala usimdharau mama yako akizeeka.

23. Nunua ukweli, wala usiuuze;nunua hekima, mafunzo na busara.

24. Baba wa mtoto mwadilifu atajaa furaha;anayemzaa mtoto mwenye hekima atamfurahia.

25. Wafurahishe baba na mama yako;mama aliyekuzaa na afurahi.

- 17 -

26. Mwanangu, nisikilize kwa makini,shikilia mwenendo wa maisha yangu.

27. Malaya ni shimo refu la kutega watu;mwanamke mgeni ni kama kisima chembamba.

28. Yeye hunyemelea kama mnyanganyi,husababisha wanaume wengi kukosa uaminifu.

- 18 -

29. Ni nani wapigao yowe?Ni nani wenye huzuni?Ni nani wenye ugomvi?Ni nani walalamikao?Ni nani wenye majeraha bila sababu?Ni nani wenye macho mekundu?

30. Ni wale ambao hawabanduki penye divai,wale wakaao chonjo kuonja divai iliyokolezwa.

31. Usiitamani divai hata kwa wekundu wake,hata kama inametameta katika bilauri,na kushuka taratibu unapoinywa.

32. Mwishowe huuma kama nyoka;huchoma kama nyoka mwenye sumu.

33. Macho yako yataona mauzauza,moyo wako utatoa mambo yaliyopotoka.

34. Utakuwa kama mtu alalaye katikati ya bahari,kama mtu alalaye juu ya mlingoti wa meli.