Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31

Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 22 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Afadhali kuwa na sifa nzuri kuliko mali nyingi;wema ni bora kuliko fedha au dhahabu.

2. Matajiri na maskini wana hali hii moja:Mwenyezi-Mungu ni Muumba wao wote.

3. Mtu mwangalifu huona hatari akajificha,lakini wajinga hujitokeza mbele wakaumia.

4. Ukinyenyekea na kumcha Mwenyezi-Mungu,utapata tuzo: Fanaka, heshima na uhai.

5. Njia ya waovu imejaa miiba na mitego;anayetaka kuhifadhi maisha yake ataiepa.

6. Mfunze mtoto namna ya kuishi vizuri,naye hatasahau njia hiyo hata uzeeni.

7. Tajiri humtawala maskini;mkopaji ni mtumwa wa mkopeshaji.

8. Apandaye dhuluma atavuna janga;uwezo wake wa kutenda mabaya utavunjwa.

9. Mtu mkarimu atabarikiwa,maana chakula chake humgawia maskini.

10. Mfukuze mwenye dharau na fujo itatoweka,ugomvi na matusi vitakoma.

11. Mwenye nia safi na maneno mazuri,atakuwa rafiki wa mfalme.

12. Mwenyezi-Mungu hulinda elimu ya kweli,lakini huyavuruga maneno ya waovu.

13. Mvivu husema, “Siwezi kutoka nje;kuna simba huko, ataniua!”

14. Kinywa cha mwasherati ni shimo refu;anayechukiwa na Mwenyezi-Mungu atatumbukia humo.

15. Mtoto hupenda mambo ya kijinga moyoni,lakini fimbo ya nidhamu humwondolea hayo.

16. Anayemdhulumu maskini atamfanya afaidike mwishowe,anayewapa matajiri zawadi ataishia kuwa maskini.

Misemo thelathini ya wenye hekima

17. Tega sikio usikie maneno ya wenye hekima,elekeza moyo wako uzingatie maarifa yangu.

18. Wewe utafurahi endapo utayaweka moyoni,na kuyakariri kila wakati.

19. Ninayependa kumfundisha leo ni wewe,ili tegemeo lako liwe kwa Mwenyezi-Mungu.

20. Nimekuandikia misemo thelathini,misemo ya maonyo na maarifa,

21. ili kukufundisha yaliyo sawa na kweli;na mtu akikuuliza uweze kumpa jibu sahihi.

- 1 -

22. Usimdhulumu maskini kwa kuwa ni maskini,wala usimnyime fukara haki yake mahakamani.

23. Maana Mwenyezi-Mungu atawatetea;atawapokonya maisha yao wale watakaowadhulumu.

- 2 -

24. Usifanye urafiki na mtu wa hasira,wala usiandamane na mwenye ghadhabu,

25. usije ukajifunza mwenendo wake,ukajinasa kabisa katika mtego.

- 3 -

26. Usiwe mmoja wao wenye kuweka ahadi,watu ambao hujiweka wadhamini wa madeni.

27. Ikiwa huna chochote cha kulipa,hata kitanda unacholalia kitachukuliwa!

- 4 -

28. Usiondoe alama ya mipaka ya zamaniambayo iliwekwa na wazee wako.