Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 41 Biblia Habari Njema (BHN)

1. “Yeyote anayeliona hilo dude,hufa moyo na kuzirai.

2. Hakuna mtu yeyote mkali athubutuye kulishtua.Nani, basi awezaye kusimama mbele yangu?

3. Nani aliyenipa kitu, ili nitakiwe kumrudishia?Chochote kilicho chini ya mbingu ni changu.

4. “Sitaacha kukueleza juu ya viungo vya hilo dudeau juu ya nguvu zake na umbo lake zuri.

5. Nani awezaye kumbambua vazi lake la nje?Nani awezaye kutoboa deraya lililovaa?

6. Nani awezaye kufungua kinywa chake?Meno yake pande zote ni kitisho!

7. Mgongo wake umefanywa kwa safu za ngaozilizoshikamana pamoja kama kwa mhuri,

8. Kila moja imeshikamana na nyingine,hata hewa haiwezi kupenya katikati yake.

9. Yameunganishwa pamoja,hata haiwezekani kuyatenganisha.

10. Likipiga chafya, mwanga huchomoza,macho yake humetameta kama jua lichomozapo.

11. Kinywani mwake hutoka mienge iwakayo,cheche za moto huruka nje.

12. Puani mwake hufuka moshi,kama vile chungu kinachochemka;kama vile magugu yawakayo.

13. Pumzi yake huwasha makaa;mwali wa moto hutoka kinywani mwake.

14. Shingo yake ina nguvu ajabu,litokeapo watu hukumbwa na hofu.

15. Misuli yake imeshikamana pamoja,imara kama chuma wala haitikisiki.

16. Moyo wake ni mgumu kama jiwe,mgumu kama jiwe la kusagia.

17. Linapoinuka, mashujaa hushikwa na woga,kwa pigo moja huwa wamezirai.

18. Hakuna upanga uwezao kulijeruhi,wala mkuki, mshale au fumo.

19. Kwake chuma ni laini kama unyasi,na shaba kama mti uliooza.

20. Mshale hauwezi kulifanya likimbie;akitupiwa mawe ya teo huyaona kama makapi.

21. Kwake, rungu ni kama kipande cha bua,hucheka likitupiwa fumo kwa wingi.

22. Tumbo lake ni kama limefunikwa na vigae vikali;hukwaruza na kurarua udongo kama chombo cha kupuria.

23. Bahari huisukasuka kama maji yachemkayo,huifanya itoe povu kama chupa ya mafuta.

24. Lipitapo huacha nyuma alama inayongaa;povu jeupe huonekana limeelea baharini.

25. Duniani hakuna kinachofanana nalo;hilo ni kiumbe kisicho na hofu.

26. Huwaona kuwa si kitu wote wenye kiburi;hilo ni mfalme wa wanyama wote wakali.”