Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 3 Biblia Habari Njema (BHN)

MAJADILIANO YA YOBU NA RAFIKI ZAKE

Yobu analalamika

1. Hatimaye Yobu aliamua kuongea, akailaani siku aliyozaliwa.

2. Yobu akasema:

3. “Ilaaniwe siku ile niliyozaliwa;usiku ule iliposemwa, ‘Mwana amechukuliwa mimba’

4. Siku hiyo na iwe giza!Mungu juu asijishughulishe nayo!Wala nuru yoyote isiiangaze!

5. Mauzauza na giza nene yaikumbe,mawingu mazito yaifunike.Giza la mchana liitishe!

6. Usiku huo giza nene liukumbe!Usihesabiwe katika siku za mwaka,wala usitiwe katika idadi ya siku za mwezi.

7. Naam, usiku huo uwe tasa,sauti ya furaha isiingie humo.

8. Walozi wa siku waulaani,watu stadi wa kuligutua dude Lewiyathani waulaani!

9. Nyota zake za pambazuko zififie,utamani kupata mwanga, lakini usipate,wala usione nuru ya pambazuko.

10. Maana usiku huo haukulifunga tumbo la mama,wala kuficha taabu nisizione.

11. Mbona sikufa nilipozaliwa,nikatoka tumboni na kutoweka?

12. Kwa nini mama yangu alinizaa?Kwa nini nikapata kunyonya?

13. Maana ningekuwa nimezikwa, kimya;ningekuwa nimelazwa na kupumzika,

14. pamoja na wafalme na watawala wa dunia,waliojijengea upya magofu yao;

15. ningekuwa pamoja na wakuu waliokuwa na dhahabu,waliojaza nyumba zao fedha tele.

16. Au, mbona sikuwa kama mimba iliyoharibika,naam, kama mtoto aliyezaliwa mfu?

17. Huko kwa wafu waovu hawamsumbui mtu,huko wachovu hupumzika.

18. Huko wafungwa hustarehe pamoja,hawaisikii kamwe sauti ya mnyapara.

19. Wakubwa na wadogo wako huko,nao watumwa wamepata uhuru mbali na bwana zao.

20. Ya nini kumjalia nuru yule aliye taabuni;na uhai yule aliye na huzuni moyoni?

21. Mtu atamaniye kifo lakini hafi;hutafuta kifo kuliko hazina iliyofichika.

22. Mtu kama huyo atashangilia mno na kufurahi,atafurahi atakapokufa na kuzikwa!

23. Ya nini kumjalia uhai mtu ambaye njia zake zimefungwa,mtu ambaye Mungu amemwekea kizuizi?

24. Kwa maana kusononeka ndio mkate wangu,kupiga kite kwangu kunatiririka mithili ya maji.

25. Kile ninachokiogopa kimenipata,ninachokihofia ndicho kilichonikumba.

26. Sina amani wala utulivu;sipumziki, taabu imenijia.”