Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 12 Biblia Habari Njema (BHN)

Jibu la Yobu

1. Ndipo Yobu akajibu:

2. “Sawa! Nyinyi ni watu wa hekima.Hekima itakufa wakati ule mtakapokufa.

3. Mimi nami ni mwelewa kama nyinyi.Mimi si mtu duni kuliko nyinyi.Yote mliyosema kila mtu anajua.

4. Nimekuwa kichekesho kwa rafiki zangu:Mimi niliyemwomba Mungu na akanijibu;mimi niliye mwadilifu na bila lawama,nimekuwa kichekesho kwa watu.

5. Mtu anayestarehe hudharau msiba;kwake, msiba huwajia wale wanaoteleza.

6. Makao ya wanyanganyi yana amani;wenye kumchokoza Mungu wako salama,nguvu yao ni mungu wao.

7. Lakini waulize wanyama nao watakufunza;waulize ndege nao watakuambia.

8. Au iulize mimea nayo itakufundisha;sema na samaki nao watakuarifu.

9. Nani kati ya viumbe hivyo,asiyejua kwamba Mwenyezi-Mungu ametenda hayo?

10. Uhai wa kila kiumbe hai umo mikononi mwake;kadhalika na pumzi ya uhai wa binadamu.

11. Je, sikio haliyapimi manenokama ulimi uonjavyo chakula?

12. Hekima iko kwa watu wazee,maarifa kwao walioishi muda mrefu.

13. Lakini hekima na uwezo ni vyake Mungu,yeye ana maarifa na ujuzi.

14. Akibomoa, hakuna awezaye kujenga upya;akimfunga mtu, hakuna awezaye kumfungua.

15. Akizuia mvua, twapata ukame;akiifungulia, nchi hupata mafuriko.

16. Yeye ana nguvu na hekima;wanaodanganywa na wanaodanganya ni wake.

17. Huwaacha washauri waende zao uchi,huwafanya waamuzi kuwa wapumbavu.

18. Huwavua wafalme vilemba vyao;na kuwafunga viunoni kamba za wafungwa;

19. Huwaacha makuhani waende uchi;na kuwaangusha wenye nguvu.

20. Huwanyanganya washauri kipawa chao cha kuongea,huwapokonya wazee hekima yao.

21. Huwamwagia wakuu aibu,huwaondolea wenye uwezo nguvu zao.

22. Huvifunua vilindi vya giza,na kuleta mwangani yaliyokuwa gizani.

23. Huyakuza mataifa kisha huyaangamiza,huyafanya yapanuke kisha huyatawanya.

24. Huwaondolea viongozi wa watu ujuzi wao,huwafanya watangetange nyikani kusiko na njia,

25. wakapapasapapasa gizani kusiko na mwanga;na kuwafanya wapepesuke kama walevi.