Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 11 Biblia Habari Njema (BHN)

Hoja ya Sofari

1. Kisha Sofari, Mnaamathi, akamjibu Yobu:

2. “Je, wingi huu wa maneno uachwe tu bila kujibiwa?Je, mtu wa maneno mengi aonesha kuwa hana hatia?

3. Je, kuropoka kwako kutanyamazisha watu?Na kama ukidhihaki, je, hamna atakayekuaibisha?

4. Wewe wadai: ‘Ninachosema ni kweli,naam, sina lawama mbele ya Mungu.’

5. Laiti Mungu angefungua kinywa chakeakatoa sauti yake kukujibu!

6. Angekueleza siri za hekima,maana yeye ni mwingi wa maarifa.Jua kwamba Mungu hakuhesabu makosa yako yote.

7. “Je, unaweza kugundua siri zake Munguna kujua ukomo wake yeye Mungu mwenye nguvu?

8. Ukuu wake wapita mbingu, wewe waweza nini?Kimo chake chapita Kuzimu,wewe waweza kujua nini?

9. Ukuu huo wapita marefu ya dunia,wapita mapana ya bahari.

10. Kama Mungu akipita,akamfunga mtu na kumhukumu,nani awezaye kumzuia?

11. Mungu anajua watu wasiofaa;akiona maovu yeye huchukua hatua.

12. “Mpumbavu hawezi kuwa na maarifa,pundamwitu ni pundamwitu tu.

13. “Yobu, ukiufanya moyo wako mnyofu,utainua mikono yako kumwomba Mungu!

14. Kama una uovu, utupilie mbali.Usikubali ubaya uwemo nyumbani mwako.

15. Hapo utajitokeza mbele ya watu bila lawama,utakuwa thabiti bila kuwa na hofu.

16. Utazisahau taabu zako zote;utazikumbuka tu kama mafuriko yaliyopita.

17. Maisha yako yatangaa kuliko jua la adhuhuri,giza lake litabadilika kuwa mngao wa pambazuko.

18. Utakuwa na ujasiri maana lipo tumaini;utalindwa na kupumzika salama.

19. Utalala bila kuogopeshwa na mtu;watu wengi watakuomba msaada.

20. Lakini waovu macho yao yatafifia,njia zote za kutorokea zitawapotea;tumaini lao la mwisho ni kukata roho!”