Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 38 Biblia Habari Njema (BHN)

Mungu anamjibu Yobu

1. Hapo Mwenyezi-Mungu alimjibu Yobu kutoka dhoruba:

2. “Nani wewe unayevuruga mashauri yangukwa maneno yasiyo na akili?

3. Jikaze kama mwanamume,nami nitakuuliza nawe utanijibu.

4. “Ulikuwa wapi nilipoiweka misingi ya dunia?Niambie, kama una maarifa.

5. Ni nani aliyeweka vipimo vyake, wajua bila shaka!Au nani aliyelaza kamba juu yake kuipima?

6. Je, nguzo za dunia zimesimikwa juu ya nini,au nani aliyeliweka jiwe lake la msingi,

7. nyota za asubuhi zilipokuwa zikiimba pamoja,na wana wa Mungu wakapaza sauti za shangwe?

8. Ni nani aliyeyafunga mafuriko ya bahariwakati yalipozuka na kuvuma kutoka vilindini?

9. Mimi ndiye niliyeifunika bahari kwa mawinguna kuiviringishia giza nene.

10. Niliiwekea bahari mipaka,nikaizuia kwa makomeo na milango,

11. nikaiambia: ‘Mwisho wako ni hapa, si zaidi!Mawimbi yako ya nguvu yatakomea hapa!’

12. “Yobu, tangu uzaliwe umewahi kuamuru kupambazuke?na kulifanya pambazuko lijue mahali pake,

13. ili lipate kuikamata dunia kwa pembe zakena kuwatimulia mbali waovu waliomo?

14. Dunia hugeuka na kupata rangi kama vazi;kama udongo wa mfinyanzi unavyogeuzwa na mhuri.

15. Lakini waovu watanyimwa mwanga wao,mkono wanaonyosha kupiga watu utavunjwa.

16. “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari?au kutembea juu ya sakafu ya kilindi cha bahari?

17. Je, umewahi kuoneshwa malango ya kifo,au kuyaona malango ya makazi ya giza nene?

18. Je, wajua ukubwa wa dunia?Niambie kama unajua haya yote.

19. “Je, makao ya mwanga yako wapi?Nyumbani kwa giza ni wapi,

20. ili upate kulipeleka kwenye makao yake,na kuifahamu njia ya kwenda huko kwake.

21. Wewe unapaswa kujua,wewe ambaye umekwisha ishi miaka mingi!

22. “Je, umewahi kuingia katika bohari za theluji,au kuona bohari za mvua ya mawe

23. ambavyo nimevihifadhi kwa ajili ya wakati wa fujo,kwa ajili ya siku ya mapigano na vita?

24. Ipi njia ya kwenda mahali mwanga unapogawanywa,au huko kunakotoka upepo wa mashariki ukasambazwa duniani?

25. “Nani aliyechora angani njia kwa ajili ya mvua?Nani aliyeionesha radi njia yake mawinguni,

26. ikasababisha mvua kunyesha nchini kusikoishi mtuna jangwani ambako hakuna mtu,

27. ili kuiburudisha nchi kavu na kamena kuifanya iote nyasi?

28. “Je, mvua ina baba?Au nani ameyazaa matone ya umande?

29. Je, barafu ilitoka tumboni kwa nani?Nani aliyeizaa theluji?

30. Maji hugeuka kuwa magumu kama jiwe,na uso wa bahari ukaganda.

31. “Angalia makundi ya nyota:Je, unaweza kuifunga minyororo Kilimia,au kuvilegeza vifungo vya Orioni?

32. Je, waweza kuziongoza nyota katika majira yake,au kumwongoza Dubu pamoja na watoto wake?

33. Je, wazijua kanuni zinazotawala mbingu;Je, waweza kuzipangia taratibu zao duniani?

34. “Je, waweza kupaza sauti na kuyaamuru mawinguyakufunike kwa mtiririko wa mvua?

35. Je, wewe ukiamuru umeme umulike,utakujia na kusema: ‘Nipo hapa?’

36. Ni nani aliyemjulisha kwarara kujaa kwa mto Niliau aliyemwambia jogoo kwamba mvua inakuja?

37. Nani mwenye akili ya kuweza kuhesabu mawingu,au kuinamisha viriba vya maji huko mbinguni?

38. ili vumbi duniani igandamanena udongo ushikamane na kuwa matope?

39. “Je, waweza kumwindia simba mawindo yakeau kuishibisha hamu ya wana simba;

40. wanapojificha mapangoni mwao,au kulala mafichoni wakiotea?

41. Ni nani awapaye kunguru chakula chao,makinda yao yanaponililia mimi Mungu,na kurukaruka huku na huko kwa njaa?