Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8

Agano la Kale

Agano Jipya

Wimbo Ulio Bora 2 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mimi ni ua la Sharoni,ni yungiyungi ya bondeni.

Bwana arusi

2. Kama yungiyungi kati ya michongoma,ndivyo alivyo mpenzi wangu kati ya wasichana.

Bibi arusi

3. Kama mtofaa kati ya miti ya msituni,ndivyo alivyo mpenzi wangu kati ya wavulana.Nafurahia kuketi chini ya kivuli chake,na tunda lake tamu sana kwangu.

4. Alinichukua hadi ukumbi wa karamu,akatweka bendera ya mapenzi juu yangu.

5. Nishibishe na zabibu kavu,niburudishe kwa matofaa,maana naugua kwa mapenzi!

6. Mkono wake wa kushoto chini ya kichwa changu,mkono wake wa kulia wanikumbatia.

7. Nawasihi enyi wanawake wa Yerusalemu,kama walivyo paa au swala wa porini,msiyachochee wala kuyaamsha mapenzi,hadi hapo wakati wake utakapofika.

Bibi arusi

Shairi la pili

8. Hiyo ni sauti ya mpenzi wangu,yuaja mbio,anaruka milima,vilima anavipita kasi!

9. Mpenzi wangu ni kama paa,ni kama swala mchanga.Amesimama karibu na ukuta wetu,achungulia dirishani,atazama kimiani.

10. Mpenzi wangu aniambia:“Inuka basi, ewe mpenzi wangu, unipendezaye,njoo twende zetu.

Bwana arusi

11. Tazama, majira ya baridi yamepita,nazo mvua zimekwisha koma;

12. maua yamechanua kila mahali.Wakati wa kuimba umefika;sauti ya hua yasikika mashambani mwetu.

13. Mitini imeanza kuzaa;na mizabibu imechanua;inatoa harufu nzuri.Njoo, basi, ewe mpenzi wangu unipendezaye,njoo twende.

14. Ee hua wangu, uliyejificha miambani.Hebu niuone uso wako,hebu niisikie sauti yako,maana sauti yako yapendeza na uso wako wavutia.

15. “Tukamatieni mbweha,wale mbweha wadogowadogo,wanaoiharibu mizabibu yetu inayochanua.”

Bibi arusi

16. Mpenzi wangu ni wangu, nami ni wake.Yeye hulisha kondoo wake penye yungiyungi,

17. hadi hapo jua linapochomozana vivuli kutoweka.Rudi kama paa mpenzi wangu,kama swala mdogo juu ya milima ya Betheri.